< Isaya 27 >

1 Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
In that day the Lord with his sore and great and mightie sword shall visite Liuiathan, that pearcing serpent, euen Liuiathan, that crooked serpent, and he shall slay the dragon that is in the sea.
2 Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
In that daye sing of the vineyarde of redde wine.
3 Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
I the Lord doe keepe it: I will water it euery moment: least any assaile it, I will keepe it night and day.
4 Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
Anger is not in mee: who would set the briers and the thornes against me in battel? I would go through them, I would burne them together.
5 Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
Or will he feele my strength, that he may make peace with me, and be at one with me?
6 Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
Hereafter, Iaakob shall take roote: Israel shall florish and growe, and the world shall be filled with fruite.
7 Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
Hath hee smitten him as hee smote those that smote him? or is hee slaine according to the slaughter of them that were slaine by him?
8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
In measure in the branches thereof wilt thou contende with it, when he bloweth with his rough winde in the day of the East winde.
9 Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
By this therefore shall the iniquitie of Iaakob be purged, and this is all the fruit, the taking away of his sinne: whe he shall make all the stones of the altars, as chalke stones broken in pieces, that the groues and images may not stand vp.
10 Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
Yet the defenced citie shalbe desolate, and the habitation shalbe forsaken, and left like a wildernes. There shall the calfe feede, and there shall he lie, and consume the branches thereof.
11 Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
When the boughes of it are drie, they shalbe broken: the women come, and set them on fire: for it is a people of none vnderstading: therefore hee that made them, shall not haue compassion of them, and he that formed them, shall haue no mercie on them.
12 Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
And in that day shall the Lord thresh from the chanell of the Riuer vnto the riuer of Egypt, and ye shalbe gathered, one by one, O children of Israel.
13 Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
In that day also shall the great trumpet be blowen, and they shall come, which perished in the land of Asshur: and they that were chased into the lande of Egypt, and they shall worship the Lord in the holy Mount at Ierusalem.

< Isaya 27 >