< Isaya 27 >

1 Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
In that day Jehovah with his hard and great and strong sword will punish leviathan the swift serpent, and leviathan the crooked serpent, and he will kill the monster that is in the sea.
2 Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
In that day is a vineyard of wine. Sing ye to it.
3 Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
I Jehovah am its keeper, I will water it every moment. Lest any hurt it, I will guard it night and day.
4 Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
Wrath is not in me. Would that the briers and thorns were against me in battle! I would march upon them. I would burn them together.
5 Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
Or else let him take hold of my strength, that he may make peace with me. Yea, let him make peace with me.
6 Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
In days to come Jacob shall take root; Israel shall blossom and bud. And they shall fill the face of the world with fruit.
7 Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
Has he smitten them as he smote those who smote them? Or are they slain according to the slaughter of those who were slain by them?
8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
In measure, in sending it forth, thou contend with it. He has removed with his rough blast in the day of the east wind.
9 Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
Therefore by this the iniquity of Jacob shall be forgiven. And this is all the fruit of taking away his sin: that he makes all the stones of the altar as chalkstones that are beaten apart, so that the Asherim and the sun-images shall rise no more.
10 Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
For the fortified city is solitary, a habitation deserted and forsaken like the wilderness. There the calf shall feed, and there he shall lie down, and consume the branches of it.
11 Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
When the boughs of it are withered, they shall be broken off. The women shall come, and set them on fire, for it is a people of no understanding. Therefore he who made them will not have compassion upon them, and he who formed them will show them no favor.
12 Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
And it shall come to pass in that day, that Jehovah will beat off his fruit, from the flood of the River to the brook of Egypt. And ye shall be gathered one by one, O ye sons of Israel.
13 Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
And it shall come to pass in that day, that a great trumpet shall be blown. And they shall come who were ready to perish in the land of Assyria, and those who were outcasts in the land of Egypt. And they shall worship Jehovah in the holy mountain at Jerusalem.

< Isaya 27 >