< Isaya 26 >

1 Katika siku ile, wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: Tuna mji ulio na nguvu, Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake.
Hiche nikho teng leh Judah gamsung cheng mijousen hiche la hi asah diu ahi: Ka khopiu hi dettah ahi! Pathen mi huhhingna banghon eium kim velun ahi.
2 Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, taifa lile lidumishalo imani.
Michonpha hodin kotpi hon peh un; tahsan umtah ho chu lut sah un.
3 Utamlinda katika amani kamilifu yeye ambaye moyo wake ni thabiti kwa sababu anakutumaini wewe.
Nangma tahsan ho jouse, lungmong sel'a nakoiding ahin, alunggel jouse nachunga koidet ho chu.
4 Mtumaini Bwana milele, kwa kuwa Bwana, Bwana, ni Mwamba wa milele.
Pakai chu tahsan jing jengun, ajehchu Pakai Pathen chu tonsot songpi ahi.
5 Huwashusha wale wajikwezao, huushusha chini mji wenye kiburi, huushusha hadi ardhini na kuutupa chini mavumbini.
Mi kiletsah ho chu asunem jin, khopi kiletsah chu asu lhujin, leivui asojin ahi.
6 Miguu huukanyaga chini, miguu ya hao walioonewa, hatua za hao maskini.
Mivaicha leh suh genthei a umhon akengtou vin achot phaovin, genthei vaichaho achunga avah leu vin ahi.
7 Mapito ya wenye haki yamenyooka. Ewe uliye Mwenye Haki, waisawazisha njia ya mtu mnyofu.
Ahin, michonpha hodin lampi chu aken pon, ajot hahpoije. Thildih jengbol Pathen chu nahin, amalam u lampi nam pet in nalhai.
8 Naam, Bwana, tukienenda katika sheria zako, twakungojea wewe, jina lako na sifa zako ndizo shauku za mioyo yetu.
Pakai, na danthu ho kanit uhin katahsan nao aphongdoh in, namin loupi ding hi kalung ngaichat pennu ahi.
9 Nafsi yangu yakutamani wakati wa usiku, wakati wa asubuhi roho yangu yakuonea shauku. Wakati hukumu zako zinapokuja juu ya dunia, watu wa ulimwengu hujifunza haki.
Jan khovah in nangma kaholjin; jingkah teng gunchu tah in Pathen kahol ji. Ajehchu leiset thutanna nahung teng lebou, miten adih chu ahet diu ahi.
10 Ingawa neema yaonyeshwa kwa waovu, hawajifunzi haki, hata katika nchi ya unyofu huendelea kutenda mabaya wala hawazingatii utukufu wa Bwana.
Migiloute nangai lut nan thilpha aboldoh deh pouve. Midangin thilpha abol vang'in, migilouten thildih lou abol jingu vin, Pakai loupina chu hetphah in aneipouve.
11 Ee Bwana, mkono wako umeinuliwa juu, lakini hawauoni. Wao na waone wivu wako kwa ajili ya watu wako tena waaibishwe, moto uliowekwa akiba kwa ajili ya adui zako na uwateketeze.
Aw Pakai na khuttum dopsang eman agel pou ve. Na mite na huhdoh nomdan chu musah in, chuteng amaho chu jachatna dimdiu ahitai. Na meikong chun nagalmi ho sumang jeng hen
12 Bwana, unaamuru amani kwa ajili yetu, yale yote tuliyoweza kuyakamilisha ni wewe uliyetenda kwa ajili yetu.
Pakai chamna neipeh diu ahi; kabol ka suh bulhit jouseu hi nang jal'a bou ahi.
13 Ee Bwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametutawala, lakini jina lako pekee ndilo tunaloliheshimu.
Aw Pakai ka Pathen u, midang hon kachung uva vai ahin hom uve, ahin nangma bou nahi keima hon ka hou uchu.
14 Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai, roho za waliokufa hazitarudi tena. Uliwaadhibu na kuwaangamiza, umefuta kumbukumbu lao lote.
Kana jen leuho chu athiuvin, aum gam tapouve. A lhagao dalhah hou hung kile talou hel ding ahi! Nangman nasat nin, na sumang gamtai. Amaho chu sottahpi gelphah louvin aumtauve.
15 Umeliongeza hilo taifa, Ee Bwana, umeliongeza hilo taifa. Umejipatia utukufu kwa ajili yako mwenyewe, umepanua mipaka yote ya nchi.
Aw Pakai, kanam u nei semlet peh taove; lentah nei so tao vin ahi. Ka gamgi hou jong nei kehlet peh un, loupina nangma kahin peuvin ahi!
16 Bwana, walikujia katika taabu yao, wewe ulipowarudi, waliweza kuomba kwa kunongʼona tu.
Pakai, lung genthei in nangma kana hol ui. Na thunun pohgihna nanoija kahungtao uve.
17 Kama mwanamke mwenye mimba aliyekaribia kuzaa anavyogaagaa na kulia kwa ajili ya maumivu yake, ndivyo tulivyokuwa mbele zako, Ee Bwana.
Numei naovop in nao anei na'a na asah a, apenchoi choi banga, Pakai, na umna'a kaum tenguleh kachuti jiu ve.
18 Tulikuwa na mimba, tuligaagaa kwa maumivu, lakini tulizaa upepo. Hatukuleta wokovu duniani, hatujazaa watu katika ulimwengu huu.
Keiho jong lungna in kijel chot chot in ka umun, ahin kagenthei thoh ujong mohseh ahi. Leiset adin huhhingna kape thei pouve, hinna jong vannoi a kapolut thei pouvin ahi.
19 Lakini wafu wenu wataishi, nayo miili yao itafufuka. Ninyi mnaokaa katika mavumbi, amkeni mkapige kelele kwa furaha. Umande wenu ni kama umande wa asubuhi, dunia itawazaa wafu wake.
Ahin Pakai a thiho chu hung hing diu, atahsau hung thoudoh kit ding ahi! Leiset a imu hochu hungthoudoh diu chuleh kipa jal'a la asah diu ahi. Ajeh chu na hinna-vah kipa chu jingkah daitwi alhah banga namite thi umna munna hunglha ding ahi.
20 Nendeni, watu wangu, ingieni vyumbani mwenu na mfunge milango nyuma yenu, jificheni kwa kitambo kidogo mpaka ghadhabu yake ipite.
In na cheuvin, kamite, na kot hou kam tup un! Chomkhat adin kisel mangun, Pakai lunghanna akichai masang sen.
21 Tazama, Bwana anakuja kutoka makao yake ili kuwaadhibu watu wa dunia kwa ajili ya dhambi zao. Dunia itadhihirisha umwagaji damu juu yake, wala haitaendelea kuwaficha watu wake waliouawa.
Ven! Leiset mite a chonset jeh un, gotna pedin Pakai chu van'a konin ahungin ahi. Leiset in akithat ho asel jou tah lou ding, mijouse mudinga hung kipuidoh diu ahi.

< Isaya 26 >