< Isaya 25 >

1 Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
Seigneur, vous êtes mon Dieu, je vous exalterai, je louerai votre nom, parce que vous avez fait des merveilles, que vous avez fidèlement accompli vos desseins anciens. Amen.
2 Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, mji wenye ngome kuwa magofu, ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, wala hautajengwa tena kamwe.
Vous avez réduit une cité en un monceau de pierres, une ville puissante en une ruine; vous avez fait que la maison des étrangers ne soit pas une cité, et que jamais elle ne soit rebâtie.
3 Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.
C’est pour cela qu’un peuple puissant vous louera, qu’une cité de nations redoutables vous craindra.
4 Umekuwa kimbilio la watu maskini, kimbilio la mhitaji katika taabu yake, hifadhi wakati wa dhoruba na kivuli wakati wa hari. Kwa maana pumzi ya wakatili ni kama dhoruba ipigayo ukuta
Parce que vous êtes devenu une force pour le pauvre, une force pour l’indigent dans sa tribulation, un espoir contre la tempête, un ombrage contre la grande chaleur; car l’esprit des violents est de même qu’un tourbillon qui fond sur une muraille.
5 na kama joto la jangwani. Wewe wanyamazisha makelele ya wageni; kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.
Comme une grande chaleur dans la soif, vous humilierez l’insolence tumultueuse des étrangers; et comme par la chaleur brûlante du soleil sous un nuage, vous ferez sécher la race des puissants.
6 Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
Et le Seigneur des armées fera à tous les peuples sur cette montagne un festin de viandes grasses, un festin de vin, de viandes moelleuses, d’un vin pur de toute he.
7 Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,
Il jettera sur cette montagne la chaîne même qui hait tous les peuples, et la toile qu’il avait ourdie pour envelopper toutes les nations.
8 yeye atameza mauti milele. Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. Bwana amesema hili.
Il précipitera la mort pour jamais; et il enlèvera, le Seigneur Dieu, les larmes de toute face, et il enlèvera l’opprobre de son peuple de la terre entière; parce que le Seigneur a parlé.
9 Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
Et son peuple dira en ce jour-là: Voici, c’est notre Dieu, celui-ci; nous l’avons attendu et il nous sauvera; c’est le Seigneur, nous l’avons attendu patiemment, nous exulterons, et nous nous réjouirons dans son salut.
10 Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu, bali Moabu atakanyagwa chini kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.
Parce que la main du Seigneur se reposera sur cette montagne, et Moab sera brisé sous lui, comme sont brisées des pailles par un chariot.
11 Watakunjua mikono yao katikati yake, kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. Mungu atashusha kiburi chao licha ya ujanja wa mikono yao.
Et il étendra ses mains sous lui, comme les étend celui qui nage pour nager; et il humiliera sa gloire, en brisant ses mains.
12 Atabomoa kuta ndefu za maboma yako na kuziangusha chini, atazishusha chini ardhini, mpaka mavumbini kabisa.
Les remparts de tes hautes montagnes s’écrouleront, et ils seront abattus et renversés par terre jusque dans la poussière.

< Isaya 25 >