< Isaya 25 >

1 Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
Yahvé, tu es mon Dieu. Je t'exalte! Je louerai ton nom, car tu as fait des choses merveilleuses, des choses prévues depuis longtemps, en toute fidélité et vérité.
2 Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, mji wenye ngome kuwa magofu, ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, wala hautajengwa tena kamwe.
Car tu as fait d'une ville un monceau, d'une ville fortifiée une ruine, d'un palais d'étrangers une ville qui n'existe plus. Elle ne sera jamais bâtie.
3 Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.
C'est pourquoi un peuple fort te glorifiera. Une ville de nations puissantes te craindra.
4 Umekuwa kimbilio la watu maskini, kimbilio la mhitaji katika taabu yake, hifadhi wakati wa dhoruba na kivuli wakati wa hari. Kwa maana pumzi ya wakatili ni kama dhoruba ipigayo ukuta
Car tu as été un refuge pour le pauvre, une forteresse pour l'indigent dans sa détresse, un abri contre la tempête, une ombre contre la chaleur, quand le souffle des redoutables est comme une tempête contre la muraille.
5 na kama joto la jangwani. Wewe wanyamazisha makelele ya wageni; kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.
Comme la chaleur d'un lieu sec, tu feras tomber le bruit des étrangers; comme la chaleur à l'ombre d'un nuage, tu feras tomber le chant des redoutables.
6 Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
Dans cette montagne, l'Éternel des armées fera à tous les peuples un festin de viandes de choix, un festin de vins de choix, de viandes de choix pleines de mœlle, de vins de choix bien raffinés.
7 Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,
Il détruira dans cette montagne la surface de la couverture qui recouvre tous les peuples, et le voile qui s'étend sur toutes les nations.
8 yeye atameza mauti milele. Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. Bwana amesema hili.
Il a englouti la mort pour toujours! Le Seigneur Yahvé essuiera les larmes de tous les visages. Il enlèvera l'opprobre de son peuple de toute la terre, car Yahvé l'a dit.
9 Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
En ce jour-là, on dira: « Voici notre Dieu! Nous l'avons attendu, et il nous a sauvés! C'est Yahvé! Nous l'avons attendu. Nous nous réjouirons et nous nous réjouirons de son salut! »
10 Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu, bali Moabu atakanyagwa chini kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.
Car la main de Yahvé s'arrêtera sur cette montagne. Moab sera foulé à sa place, comme on foule la paille dans l'eau du fumier.
11 Watakunjua mikono yao katikati yake, kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. Mungu atashusha kiburi chao licha ya ujanja wa mikono yao.
Il étendra ses mains au milieu d'elle, comme celui qui nage étend ses mains pour nager, mais son orgueil sera humilié avec l'art de ses mains.
12 Atabomoa kuta ndefu za maboma yako na kuziangusha chini, atazishusha chini ardhini, mpaka mavumbini kabisa.
Il a abattu la haute forteresse de tes murs, il l'a abaissée, il l'a ramenée à terre, jusqu'à la poussière.

< Isaya 25 >