< Isaya 25 >

1 Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
HERRE, min Gud er du; jeg priser dig, lover dit Navn. Thi du har gjort et Under, Raad fra fordum var tro og sande.
2 Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, mji wenye ngome kuwa magofu, ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, wala hautajengwa tena kamwe.
Thi du lagde Byen i Grus, den faste Stad i Ruiner; de fremmedes Borg er nedbrudt, aldrig mer skal den bygges.
3 Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.
Derfor ærer dig et mægtigt Folk, frygter dig grumme Hedningers Stad.
4 Umekuwa kimbilio la watu maskini, kimbilio la mhitaji katika taabu yake, hifadhi wakati wa dhoruba na kivuli wakati wa hari. Kwa maana pumzi ya wakatili ni kama dhoruba ipigayo ukuta
Thi du blev de ringes Værn, den fattiges Værn i Nøden, et Ly mod Skylregn, en Skygge mod Hede; thi som isnende Regn er Voldsmænds Aande,
5 na kama joto la jangwani. Wewe wanyamazisha makelele ya wageni; kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.
som Hede i det tørre Land. Du kuer de fremmedes Larm; som Hede ved Skyens Skygge saa dæmpes Voldsmænds Sang.
6 Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
Hærskarers HERRE gør paa dette Bjerg et Gæstebud for alle Folkeslag med fede Retter og stærk Vin, med fede, marvfulde Retter og stærk og klaret Vin.
7 Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,
Og han borttager paa dette Bjerg Sløret, som tilslører alle Folkeslag, og Dækket, der dækker alle Folk.
8 yeye atameza mauti milele. Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. Bwana amesema hili.
Han opsluger Døden for stedse. Og den Herre HERREN aftørrer Taaren af hver en Kind og gør Ende paa sit Folks Skam paa hele Jorden, saa sandt HERREN har talet.
9 Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
Paa hin Dag skal man sige: Se, her er vor Gud, som vi biede paa, og som frelste os; her er HERREN, som vi biede paa. Lad os juble og glæde os over hans Frelse;
10 Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu, bali Moabu atakanyagwa chini kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.
thi HERRENS Haand hviler over dette Bjerg. Men Moab trampes ned, hvor det staar, som Straa i Møddingpølen;
11 Watakunjua mikono yao katikati yake, kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. Mungu atashusha kiburi chao licha ya ujanja wa mikono yao.
det breder sine Hænder ud deri, som Svømmeren gør for at svømme, og han ydmyger dets Hovmod trods Hændernes Kunstgreb.
12 Atabomoa kuta ndefu za maboma yako na kuziangusha chini, atazishusha chini ardhini, mpaka mavumbini kabisa.
Han nedbryder og nedstyrter de stejle Mures Værn; han jævner dem med Jorden, saa de ligger i Støvet.

< Isaya 25 >