< Isaya 24 >

1 Tazama, Bwana ataifanya dunia kuwa ukiwa na kuiharibu, naye atauharibu uso wake na kutawanya wakaao ndani yake:
Redzi, Tas Kungs zemi dara tukšu, un to izposta un pārvērš viņas seju un izklīdina viņas iedzīvotājus.
2 ndivyo itakavyokuwa kwa makuhani na kwa watu, kwa bwana na kwa mtumishi, kwa bibi na kwa mtumishi wake wa kike, kwa muuzaji na kwa mnunuzi, kwa mkopaji na kwa mkopeshaji, kwa mdaiwa na kwa mdai.
Un kā tiem ļaudīm, tāpat klāsies priesterim; kā kalpam, tāpat viņa kungam; kā kalponei tāpat viņas saimniecei; kā pircējam, tāpat pārdevējam; kā aizdevējam, tāpat aizņēmējam; kā pagaidu dzinējam, tāpat pagaidu maksātajam.
3 Dunia itaharibiwa kabisa na kutekwa nyara kabisa. Bwana amesema neno hili.
Postīt to zemi izpostīs, un laupīt viņu izlaupīs; jo Tas Kungs šo vārdu ir runājis.
4 Dunia inakauka na kunyauka, dunia inanyongʼonyea na kunyauka, waliotukuzwa wa dunia wananyongʼonyea.
Zeme tvīkst un nīkst, zemes virsas gurst un vīst, ļaužu augstie tai zemē gurst.
5 Dunia imetiwa unajisi na watu wake; wameacha kutii sheria, wamevunja amri na kuvunja agano la milele.
Jo zeme ir sagānīta no saviem iedzīvotājiem, jo tie pārkāpj bauslību un pārgroza likumu un lauž to mūžīgo derību.
6 Kwa hiyo laana inaiteketeza dunia, watu wake lazima waichukue hatia yao. Kwa hiyo wakazi wa dunia wameteketezwa, nao waliosalia ni wachache sana.
Tādēļ lāsti zemi noēd, un kas tur dzīvo, tiem jācieš; tādēļ zemes iedzīvotāji nokalst un maz cilvēku atliks.
7 Divai mpya inakauka na mzabibu unanyauka, watu wote wafurahishao wanalia kwa huzuni.
Vīns nonīcis, vīna koks savītis, visi, kam bija priecīga sirds, nopūšas.
8 Furaha ya matoazi imekoma, kelele za wenye furaha zimekoma, shangwe za kinubi zimenyamaza.
Bungu prieks apklusis, līksmu ļaužu troksnis nostājies, kokles prieks pagalam.
9 Hawanywi tena mvinyo pamoja na wimbo, kileo ni kichungu kwa wanywaji wake.
Vīnu vairs nedzer ar dziesmām, stiprais dzēriens dzērājiem rūgts.
10 Mji ulioharibiwa umekuwa ukiwa, mlango wa kila nyumba umefungwa.
Tukša pilsēta izpostīta, visi nami aizslēgti, ka nevar ieiet.
11 Barabarani wanalilia kupata mvinyo, furaha yote imegeuka kuwa majonzi, furaha yote imefukuziwa mbali na dunia.
Vīna pēc žēlojās uz ielām, zuduši visi prieki, zemes līksmība ir projām.
12 Mji umeachwa katika uharibifu, lango lake limevunjwa vipande.
Posts vien pilsētā atlicis, un vārti salauzti drupu drupās.
13 Ndivyo itakavyokuwa duniani na miongoni mwa mataifa, kama vile wakati mzeituni upigwavyo, au kama vile wakati masazo yabakiavyo baada ya zabibu kuvunwa.
Jo tā notiks pa zemes virsu tautu starpā, kā kad eļļas koku nokrata, tā kā kad atlikas lasa pēc ķekaru noņemšanas.
14 Wanainua sauti zao, wanapiga kelele kwa furaha, kutoka magharibi wanasifu kwa ukelele utukufu wa Bwana.
Tie paceļ savu balsi un dzied priecīgi, pār Tā Kunga godību tie gavilē no jūras puses.
15 Kwa hiyo upande wa mashariki mpeni Bwana utukufu, liadhimisheni jina la Bwana, Mungu wa Israeli, katika visiwa vya bahari.
Tādēļ godinājiet To Kungu austruma zemē, tais jūras salās Tā Kunga, Israēla Dieva, vārdu.
16 Kutoka miisho ya dunia tunasikia uimbaji: “Utukufu kwa Yule Mwenye Haki.” Lakini nilisema, “Ninadhoofika, ninadhoofika! Ole wangu! Watenda hila wanasaliti! Kwa hila watenda hila wanasaliti!”
No zemes gala mēs dzirdam dziesmas par godu tam taisnam. Bet man jāsaka: nelaime, nelaime, ak vai, man! Laupītāji laupa, laupīdami laupa laupītāji.
17 Hofu, shimo na mtego vinakungojea, ewe mtu ukaaye duniani.
Briesmas un bedre un valgs pār tevi, tu zemes iedzīvotājs!
18 Kila akimbiaye asikiapo sauti ya hofu atatumbukia shimoni, naye yeyote apandaye kutoka shimoni, atanaswa kwenye mtego. Malango ya gharika ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.
Kas no briesmu balss izbiedēts bēgs, tas kritīs bedrē, un kas no bedres izkāps, tas taps sagūstīts valgā. Jo augstības logi atvērti un zemes pamati trīc.
19 Dunia imepasuka, dunia imechanika, dunia imetikiswa kabisa.
Zeme sprāgdama sprāgs, zeme plīsdama plīsīs, zeme trīcēdama trīcēs,
20 Dunia inapepesuka kama mlevi, inayumbayumba kama kibanda kwenye upepo; imelemewa sana na mzigo wa hatia ya uasi wake na ikianguka kamwe haitainuka tena.
Zeme streipuļos kā piedzēris vīrs un šūposies kā šūpulis, un viņas grēki uz viņas būs smagi, un viņa kritīs un necelsies vairs augšām.
21 Katika siku ile Bwana ataadhibu nguvu zilizoko mbinguni juu, na wafalme walioko duniani chini.
Un tai dienā Tas Kungs piemeklēs to augstības karaspēku augstībā un tos zemes ķēniņus virs zemes.
22 Watakusanywa pamoja kama wafungwa waliofungwa gerezani, watafungiwa gerezani na kuadhibiwa baada ya siku nyingi.
Un tie taps ieslodzīti kā cietumnieki bedrē, un taps saslēgti cietumā, un pēc ilga laika tie atkal taps piemeklēti.
23 Mwezi utatiwa haya, nalo jua litaaibishwa; kwa maana Bwana Mwenye Nguvu Zote atawala juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu, tena mbele ya wazee wake kwa utukufu.
Un mēnesis nosarks, un saule nobālēs, jo Tas Kungs Cebaot ir ķēniņš Ciānas kalnā un Jeruzālemē, un viņas vecaju priekšā būs godība.

< Isaya 24 >