< Isaya 23 >

1 Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
Sur Kenti'yle ilgili bildiri: Ey ticaret gemileri, feryat edin! Çünkü Sur Kenti evleriyle, Limanlarıyla birlikte yok oldu. Kittim'den size haber geldi.
2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
Ey kıyı halkı ve denizcilerin zenginleştirdiği Sayda tüccarları, susun!
3 Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
Şihor'un tahılı, Nil'in ürünü Denizleri aşar, Sur'a gelir sağlardı. Ulusların kârı ona akardı.
4 Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
Utan, ey Sayda, ey deniz kıyısındaki kale! Çünkü deniz sana sesleniyor: “Ne doğum ağrısı çektim, ne de doğurdum. Ne delikanlılar büyüttüm, ne de kızlar.”
5 Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
Sur'un haberi Mısır'a ulaşınca, Yüreği burkulacak insanların.
6 Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
Tarşiş'e geçin, ey kıyıda oturanlar, Feryat edin.
7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
Uzak ülkeleri yurt edinmiş, Eğlenceye düşkün halkınız, Eski, tarihsel kentiniz bu mu?
8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
Taçlar giydiren Sur'a karşı bu işi kim tasarladı? O kent ki, tüccarları prenslerdi, İş adamları dünyanın saygın kişileriydi.
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
Görkeminin sonucu olan gururunu kırmak, Dünyaca ünlü bütün saygın kişilerini alçaltmak için Her Şeye Egemen RAB tasarladı bunu.
10 Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
Kendi topraklarını Nil gibi basıp geç, Ey Tarşiş kızı, artık engel yok.
11 Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
RAB denizin üzerine elini uzatıp ülkeleri titretti, Kenan kalelerinin yıkılmasını buyurdu.
12 Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
“Eğlencen sona erdi, ey Sayda, erden kız!” dedi, “Kirletildin. Kalk, Kittim'e geç, Orada bile rahat yüzü görmeyeceksin.”
13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
Kildan ülkesine bak! O halk yok artık. Asurlular onların ülkesini yabanıl hayvanlara verdi, Kuşatma kuleleri diktiler, saraylarını soydular, Ülkeyi viraneye çevirdiler.
14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
Feryat edin, ey ticaret gemileri! Çünkü sığınağınız harap oldu.
15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
Bundan sonra Sur Kenti yetmiş yıl, bir kralın ömrü süresince unutulacak. Yetmiş yıl bitince, fahişe için bestelenen türküdeki gibi Sur'a şöyle denecek:
16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
“Bir lir al, dolaş kenti, Ey sen, unutulmuş fahişe! Güzel çal seni anımsamaları için, Türkü üstüne türkü söyle.”
17 Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
Yetmiş yıl geçince RAB Sur'la ilgilenecek, ama Sur para için yine fahişeliğe dönecek. Dünyanın bütün krallıklarıyla fahişelik edecek.
18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.
Kentin ticaretten ve fuhuştan kazandıkları RAB'be adanacak. Bunlar biriktirilmeyecek, hazineye konmayacak. Ticaretten kazandıklarını doyuncaya dek yesinler, güzel güzel giyinsinler diye RAB'bin önünde yaşayanlara verilecek.

< Isaya 23 >