< Isaya 23 >

1 Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
Плачитеся, корабли Кархидонстии, яко погибе, и ктому не идут от земли Китиейския, отведеся пленен.
2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
Кому подобни быша живущии во острове, купцы Финичестии, преходящии море?
3 Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
В воде мнозе семя купеческо, аки жатве вносимей купцы язычестии.
4 Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
Усрамися, Сидоне, рече море. Крепость же морская рече: не болех, ни породих, ни вскормих юнош, ниже вознесох девиц.
5 Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
Егда же слышано будет во Египте, приимет я болезнь о Тире.
6 Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
Идите в Кархидон, плачитеся, живущии во острове сем.
7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
Не сие ли бе величание вам исперва, прежде неже предану быти ему?
8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
Кто сия совеща на Тира? Еда хуждший есть, или не крепкий есть? Купцы его славнии князи земли.
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
Господь Саваоф совеща разсыпати всякую гордыню славных и обезчестити всякое славное на земли.
10 Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
Делай землю твою, ибо корабли ктому не приидут от Кархидона.
11 Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
И рука Твоя ктому не укрепеет по морю, разгневляющая царей. Господь Саваоф заповеда о Ханаане, еже погубити крепость его.
12 Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
И рекут: ктому не приложите укаряти и обидети дщерь Сидоню: и аще отидеши ко Китииом, ниже тамо будет тебе покой:
13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
и в землю Халдейску, но и та опустела от Ассириан, яко стена ея падеся.
14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
Плачитеся, корабли Кархидонстии, яко погибе твердыня ваша.
15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
И будет в той день, оставлен будет Тир седмьдесят лет, якоже время (единаго) царя, яко время человеческо: и по седмидесятих летех будет Тир яко песнь блудницы.
16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
Возми гусли, обыди град, блудница забвеная, добре погуди, много воспой, да память твоя будет.
17 Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
И будет по седмидесятих летех, присещение сотворит Бог Тиру, и паки возставится на прежднее и будет торжище всем царствам вселенныя на лицы земли.
18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.
И будет его купля и мзда свято Господеви, не им собрано будет, но живущым пред Господем, вся купля его, ясти и пити и наполнитися, и в сытость, на память пред Господем.

< Isaya 23 >