< Isaya 23 >

1 Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
Malheur accablant de Tyr. Hurlez, vaisseaux de la mer, parce qu’a été dévastée la maison d’où les navires avaient accoutumé de venir; c’est de la terre de Céthim que cela leur a été révélé.
2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
Gardez le silence, vous qui habitez dans l’île; les marchands de Sidon, traversant la mer, t’ont remplie.
3 Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
Au milieu de grandes eaux la semence du Nil, la moisson du fleuve étaient ses fruits; et elle est devenue le marché des nations.
4 Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
Rougis, Sidon, car la mer parle, la force de la mer, disant: Je n’ai pas été en travail, et je n’ai pas enfanté, et je n’ai pas nourri de jeunes hommes, et je n’ai pas élevé déjeunes vierges.
5 Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
Lorsque le bruit sera parvenu en Egypte, on sera dans la douleur en apprenant la ruine de Tyr.
6 Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
Passez les mers, hurlez, vous qui habitez dans l’île:
7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
N’est-elle pas la vôtre cette ville, qui dès les anciens jours se glorifiait de son antiquité? Ses pieds la conduiront dans une terre étrangère pour demeurer.
8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
Qui a formé ce dessein contre Tyr, autrefois couronnée, dont les marchands étaient des princes, et les trafiquants des personnages illustres de la terre?
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
C’est le Seigneur des armées qui a formé ce dessein, afin d’enlever l’orgueil de toute gloire et de conduire à l’ignominie tous les illustres de la terre
10 Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
Traverse ta terre comme un fleuve, fille de la mer; il n’y a plus de ceinture pour toi.
11 Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
Le Seigneur a étendu sa main sur la mer, il a ébranlé des royaumes, il a donné ses ordres contre Chanaan, afin de briser ses vaillants guerriers.
12 Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
Et il a dit: Tu ne te glorifieras plus, souffrant violence, après ton ignominie, vierge, fille de Sidon; lève-toi, passe à Céthim, là aussi il n’a pas de repos pour toi.
13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
Voilà la terre des Chaldéens, il n’y eut point un tel peuple, Assur l’a fondée; cependant on a emmené en captivité ses hommes robustes, on a démoli ses maisons, et on en a fait des ruines.
14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
Hurlez, vaisseaux de la mer, parce que votre force est détruite.
15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
Et il arrivera en ce jour-là que tu seras dans l’oubli, ô Tyr, soixante-dix ans, comme sont les jours d’un seul roi; mais après soixante-dix ans, Tyr chantera comme une prostituée.
16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
Prends ta harpe, et parcours la ville, prostituée livrée à l’oubli; chante bien, réitère souvent ton chant, afin qu’il y ait souvenir de toi.
17 Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
Et il arrivera après soixante-dix ans, que le Seigneur visitera Tyr, et qu’il la ramènera à son commerce, et que de nouveau elle forniquera avec tous les royaumes de la terre, sur la face de la terre.
18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.
Et ses affaires et ses profits seront consacrés au Seigneur; ils ne seront pas renfermés, ni mis en réserve, parce que c’est pour ceux qui habitent devant le Seigneur, que sera leur commerce, afin qu’ils mangent à satiété, et qu’ils soient revêtus jusqu’à la vieillesse.

< Isaya 23 >