< Isaya 23 >

1 Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
[the] oracle of Tyre wail - O ships of Tarshish for it has been devastated from house from coming from [the] land of Cyprus it has been revealed to them.
2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
Be silent O inhabitants of [the] coastland [the] trader of Sidon [who] passed over [the] sea they have filled you.
3 Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
And on waters many [was] [the] seed of Shihor [the] harvest of [the] River revenue her and it became [the] traffic of nations.
4 Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
Be ashamed O Sidon for it has said [the] sea [the] stronghold of the sea saying not I have been in labor and not I have given birth and not I have brought up young men I have raised young women.
5 Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
When a report [is] to Egypt people will be in anguish like [the] report of Tyre.
6 Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
Pass over Tarshish towards wail O inhabitants of [the] coastland.
7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
¿ [is] this Of you jubilant [city] [which is] from days of antiquity beginning its [which] they have carried it feet its from a distance to sojourn.
8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
Who? did he plan this on Tyre which bestows crowns which traders its [were] princes merchants its [were the] honored [people] of [the] earth.
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
Yahweh of hosts he planned it to profane [the] pride of all splendor to treat with contempt all [the] honored [people] of [the] earth.
10 Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
Pass over land your like the River O daughter of Tarshish there not [is] a restraint still.
11 Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
Hand his he has stretched out over the sea he has made tremble kingdoms Yahweh he has commanded concerning Canaan to destroy strongholds its.
12 Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
And he said not you will repeat again to exult O oppressed [one] [the] virgin of [the] daughter of Sidon (Cyprus *Q(k)*) arise pass over also there not it will be rest to you.
13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
There! - [the] land of [the] Chaldeans this [is] the people [which] not it was Assyria it allocated it to desert-dwellers they raised up (siege-towers its *Q(k)*) they stripped bare palaces its it made it a ruin.
14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
Wail O ships of Tarshish for it has been devastated stronghold your.
15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
And it will be in the day that and [will be] forgotten Tyre seventy year[s] like [the] days of a king one from [the] end of seventy year[s] it will happen to Tyre like [the] song of the prostitute.
16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
Take a harp go around [the] city O prostitute forgotten do well to play multiply song so that you may be remembered.
17 Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
And it will be from [the] end of - seventy year[s] he will visit Yahweh Tyre and it will return to hire its and it will act [the] prostitute with all [the] kingdoms of the earth on [the] surface of the earth.
18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.
And it will be profit its and hire its a holy thing to Yahweh not it will be stored up and not it will be hoarded for to [those who] dwell before Yahweh it will belong profit its for eating to satiety and for covering magnificent.

< Isaya 23 >