< Isaya 23 >

1 Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
The burden of Tyre. Wail, you ships of the sea! For the house, from which they were accustomed to go forth, has been laid waste. From the land of Kittim, this has been revealed to them.
2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
Be silent, you inhabitants of the island! The merchants of Sidon, crossing over the sea, have filled you.
3 Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
The offspring of the Nile is in the midst of many waters. The harvest of the river is her crop. And she has become the marketplace of the nations.
4 Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
Be ashamed, O Sidon! For the sea speaks, the strength of the sea, saying: “I have not been in labor, and I have not given birth, and I have not raised young men, nor have I promoted the development of virgins.”
5 Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
When it has been heard in Egypt, they will be in anguish, when they hear of Tyre.
6 Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
Cross over the seas. Wail, you inhabitants of the island!
7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
Is this not your place, which from its earliest days has gloried in its antiquity? Her feet will lead her to a sojourn far away.
8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
Who has made this plan against Tyre, which formerly was crowned, whose merchants were leaders, whose traders were illustrious on the earth?
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
The Lord of hosts has planned this, so that he may tear down the arrogance of all glory, and may bring disgrace to all the illustrious of the earth.
10 Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
Cross through your land, as through a river, O daughter of the sea. You no longer have a belt.
11 Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
He has extended his hand over the sea. He has stirred up kingdoms. The Lord has given an order against Canaan, so that he may crush its strong.
12 Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
And he said: “You shall no longer increase so as to glory, while enduring calumny, O virgin daughter of Sidon. Rise up and set sail for Kittim; in that place, too, there will be no rest for you.”
13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
Behold, the land of the Chaldeans: never before was there such a people! Assur founded it. They have led away its strong ones into captivity. They have dug under its houses. They have left it in ruins.
14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
Wail, you ships of the sea! For your strength has been devastated.
15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
And this shall be in that day: you, O Tyre, will be forgotten for seventy years, like the days of one king. Then, after seventy years, there will be, for Tyre, something like the canticle of a harlot.
16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
Take up a stringed instrument. Circulate through the city, you harlot who had been forgotten. Sing many canticles well, so that you may be remembered.
17 Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
And this shall be after seventy years: the Lord will visit Tyre, and he will lead her back to her profits. And she will fornicate again with all the kingdoms of the world upon the face of the earth.
18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.
And her businesses and her profits will be sanctified to the Lord. They will not be locked away and they will not be stored. For her business will be for those who will live in the presence of the Lord, so that they may eat until satisfied, and may be well-clothed even into old age.

< Isaya 23 >