< Isaya 23 >

1 Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
The burden of Tyre. Howl, ye ships of Tarshish, for it is laid waste, so that there is no house, no entering in. It is revealed to them from the land of Kittim.
2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
Be still, ye inhabitants of the coast, thou whom the merchants of Sidon, who pass over the sea, have replenished.
3 Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
And on great waters the seed of the Shihor, the harvest of the Nile, was her revenue, and she was the mart of nations.
4 Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
Be thou ashamed, O Sidon, for the sea has spoken, the stronghold of the sea, saying, I have not travailed, nor brought forth, neither have I nourished young men, nor brought up virgins.
5 Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
When the report comes to Egypt, they shall be greatly pained at the report of Tyre.
6 Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
Pass ye over to Tarshish. Wail, ye inhabitants of the coast.
7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
Is this your joyous city, whose antiquity is of ancient days, whose feet carried her afar off to sojourn?
8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
Who has purposed this against Tyre, the bestower of crowns, whose merchants are rulers, whose traders are the honored of the earth?
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
Jehovah of hosts has purposed it, to stain the pride of all glory, to bring into contempt all the honorable of the earth.
10 Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
Pass through thy land as the Nile, O daughter of Tarshish, there is no restraint any more.
11 Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
He has stretched out his hand over the sea. He has shaken the kingdoms. Jehovah has given commandment concerning Canaan, to destroy the strongholds of it.
12 Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
And he said, Thou shall no more rejoice, O thou oppressed virgin daughter of Sidon. Arise, pass over to Kittim, even there shall thou have no rest.
13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
Behold, the land of the Chaldeans. This people once was not. The Assyrian founded it for those who dwell in the wilderness. They set up their towers. They raised up the palaces of it. Then they made it a ruin.
14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
Howl, ye ships of Tarshish, for your stronghold is laid waste.
15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
And it shall come to pass in that day, that Tyre shall be forgotten seventy years, according to the days of one king. After the end of seventy years it shall be to Tyre as in the song of the harlot:
16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
Take a harp, go about the city, thou harlot who has been forgotten. Make sweet melody, sing many songs, that thou may be remembered.
17 Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
And it came to pass after the end of seventy years, that Jehovah examined Tyre, and she has repented of her gift, that she play the harlot with all the kingdoms of the world upon the face of the earth.
18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.
And her merchandise and her pay shall be holiness to Jehovah. It shall not be treasured nor laid up, for her merchandise shall be for those who dwell before Jehovah, to eat sufficiently, and for durable clothing.

< Isaya 23 >