< Isaya 23 >

1 Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
Profeti imod Tyrus. Hyler, I Tharsis's Skibe! thi den er ødelagt, saa der ikke er et Hus, og saa at ingen kommer derind; fra Kithims Land kundgøres dette for dem.
2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
Tier, I Indbyggere paa Øen, som Zidons Købmænd, der fore over Havet, fyldte!
3 Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
Over de store Vande blev Sæden ved Sikor, Høsten ved Strømmen, dens Indkomst; og den var Hedningernes Stapelstad.
4 Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
Skam dig, Zidon! thi Havet, Befæstningen ved Havet, siger: Jeg har ikke været i Fødselsnød og har ikke født og ikke opdraget unge Karle og ikke opfødt Jomfruer.
5 Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
Saa si art Rygtet naar Ægypten, skulle de blive bange ved Rygtet om Tyrus.
6 Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
Farer over til Tharsis, hyler, I Indbyggere paa Øen!
7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
Er dette eders jublende Stad, den, hvis Udspring er fra Oldtid, den, hvis Fødder føre den ud, langt bort til at være fremmed?
8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
Hvo har besluttet dette over Tyrus, den, som uddelte Kroner, den, hvis Købmænd vare Fyrster, den, hvis Kræmmere vare de herligste paa Jorden?
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
Den Herre Zebaoth har besluttet det for at nedslaa al denne dejlige Herlighed, for at gøre de herlige paa Jorden ringe.
10 Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
Far igennem dit Land som Strømmen, du Tharsis's Datter! der er intet Bælte ydermere.
11 Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
Han udrakte sin Haand over Havet, han bragte Rigerne til at bæve; Herren bød om Kanaan at ødelægge dens Befæstninger.
12 Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
Og han sagde: Du skal ikke blive ved at fryde dig ydermere, du voldtagne Jomfru, Zidons Datter! gør dig rede, drag hen over til Kithim; men end ikke der skal du have Hvile.
13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
Se, Kaldæernes Land — der er Folket, som ikke længe har været til, Assur har grundlagt det for Ørkenens Børn — de have oprejst Vagttaarne, nedbrudt dens Paladser, gjort den til en Stenhob.
14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
Hyler, I Tharsis's Skibe! thi eders Befæstning er forstyrret.
15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
Og det skal ske paa den Dag, da skal Tyrus blive glemt halvfjerdsindstyve Aar, som ere en Konges Dage; men naar halvfjerdsindstyve Aar ere til Ende, skal det gaa Tyrus efter Skøgevisen:
16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
„Tag Harpe, gak omkring i Staden, du glemte Skøge! leg smukt paa Strenge, syng meget, paa det du maa ihukommes!”
17 Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
Og det skal ske, efter at halvfjerdsindstyve Aar ere til Ende, da skal Herren besøge Tyrus, og den skal komme til sin Fortjeneste igen og bole med alle Riger paa Jorden, paa Jordens Kreds.
18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.
Men dens Købmandsskab og dens Fortjeneste skal være Herren helliget, det skal ikke samles til Liggendefæ, ej heller henlægges; thi de, som bo for Herrens Ansigt, skulle have dens Købmandsskab, at de maa æde og blive mætte og kunne klæde sig herligt.

< Isaya 23 >