< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
Malheur accablant de la vallée de Vision. Qu’as-tu donc, toi aussi, que tu es montée tout entière sur les toits?
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
Pleine de clameur, ville nombreuse, cité exultante, ceux qui t’ont été tués ne sont pas des tués par le glaive, ni des morts à la guerre.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
Tous les princes ont fui ensemble, et ont été durement attachés; tous ceux qui ont été trouvés, ont été garrottés pareillement; cependant ils ont fui bien loin.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
À cause de cela j’ai dit: Retirez-vous de moi, je pleurerai amèrement; ne cherchez pas à me consoler sur la dévastation de la fille de mon peuple.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
Car c’est un jour de tuerie, de foulement aux pieds et de pleurs, jour venant du Seigneur Dieu des armées dans la vallée de Vision, examinant le mur, et fier sur la montagne.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
Et Elam a pris un carquois, le chariot du cavalier, le bouclier a laissé la muraille nue.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
Et les meilleures vallées seront remplies de quadriges, et les cavaliers mettront le siège devant les portes.
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
Et ce qui couvrait Juda sera ôté, et tu verras en ce jour-là l’arsenal de la maison de la forêt.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
Et vous verrez que les brèches de la cité de David ont été multipliées, et vous avez rassemblé les eaux de la piscine inférieure,
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
Et vous avez fait le dénombrement des maisons de Jérusalem, et vous avez détruit les maisons pour fortifier le mur.
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
Et vous avez fait un réservoir entre les deux murs, près de l’eau de la piscine ancienne, et vous n’avez pas levé les yeux vers celui qui l’avait faite, et vous n’avez pas vu même de loin celui qui l’a construite.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
Et le Seigneur Dieu des armées vous appellera en ce jour-là au pleur, au gémissement, à raser vos cheveux, et à vous ceindre d’un sac;
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
Et voici la joie et l’allégresse; tuer des veaux, égorger des béliers, manger des viandes, et boire du vin. Mangeons et buvons; car demain nous mourrons.
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
Et s’est révélée à mes oreilles la voix du Seigneur des armées: Non, elle ne vous sera pas remise, cette iniquité, jusqu’à ce que vous mouriez, dit le Seigneur Dieu des armées.
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Voici ce que dit le Seigneur Dieu des armées: Va, entre auprès de celui qui habite dans le tabernacle, auprès de Sobna, le préposé du temple, et tu lui diras:
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
Que fais-lu ici, ou à quel titre es-tu ici? que tu t’es taillé ici un sépulcre, que sur un lieu élevé tu l’es taillé dans la pierre un monument, un tabernacle.
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Voici que le Seigneur te fera transporter comme est transporté un coq, et comme un manteau, ainsi il t’enlèvera.
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
Te couronnant, il te couronnera de tribulation, il te lancera comme une balle dans une terre large et spacieuse; là tu mourras, et là sera le char de ta gloire, l’ignominie de la maison de ton Seigneur.
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
Je te chasserai de ton rang, et de ton ministère je te déposerai.
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
Et il arrivera en ce jour-là que j’appellerai mon serviteur Eliacim, fils d’Helcias,
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
Et je le revêtirai de ta tunique, je lui attacherai fortement ta ceinture, et ta puissance, je la mettrai en sa main; et il sera comme un père pour les habitants de Jérusalem et pour la maison de Juda.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
Et je mettrai la clef de la maison de David sur son épaule, et il ouvrira, et il n’y aura personne qui ferme; et il fermera, et il n’y aura personne qui ouvre.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
Et je le ficherai comme un pieu dans un lieu sûr, et il sera comme un trône de gloire pour la maison de son père.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
On y suspendra toute la gloire de la maison de son père, les divers genres de vases, tout vase le plus petit, depuis les vases cratères jusqu’à tout instrument de musique.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
En ce jour-là, dit le Seigneur des armées, sera enlevé le pieu qui avait été fiché dans un lieu sûr; et sera brisé et tombera et périra tout ce qui y avait été suspendu, parce que le Seigneur a parlé.

< Isaya 22 >