< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
Ennustus Näkylaaksosta. Mikä sinun on, kun sinä kaikkinesi katoille nouset,
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
sinä humuavainen, pauhaava kaupunki, sinä remuava kylä? Surmattusi eivät ole miekan surmaamia, eivät sotaan kuolleita.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
Kaikki sinun päämiehesi yhdessä pakenivat, joutuivat vangiksi, jousta vailla; keitä ikinä sinun omiasi tavattiin, ne vangittiin kaikki tyynni, kuinka kauas pakenivatkin.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
Sentähden minä sanon: "Kääntäkää katseenne minusta pois: minä itken katkerasti; älkää tunkeilko minua lohduttamaan, kun tytär, minun kansani, tuhoutuu".
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
Sillä hämmingin, hävityksen ja häiriön päivän on Herra, Herra Sebaot, pitävä Näkylaaksossa. Muurit murrettiin, vuorille kohosi huuto.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
Eelam nosti viinen, tullen vaunuineen, väkineen ja ratsumiehineen, ja Kiir paljasti kilven.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
Ihanimmat laaksosi täyttyivät vaunuista, ratsumiehet asettuivat asemiin portin eteen.
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
Hän riisui Juudalta verhon, ja sinä päivänä sinä loit katseesi Metsätalon asevarastoon.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
Te huomasitte monta repeämää Daavidin kaupungin muurissa ja kokositte vedet Alalammikkoon;
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
te luitte Jerusalemin talot ja hajotitte taloja vahvistaaksenne muurin,
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
ja te teitte molempien muurien välille paikan, johon Vanhan lammikon vedet koottiin. Mutta hänen puoleensa te ette katsoneet, joka tämän tuotti, häntä te ette nähneet, joka tämän kauan sitten valmisti.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
Ja sinä päivänä Herra, Herra Sebaot, kutsui itkuun ja valitukseen, pään paljaaksi ajamaan ja säkkiin vyöttäytymään.
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
Mutta katso: on ilo ja riemu, raavaitten tappaminen ja lammasten teurastus, lihan syönti ja viinin juonti! "Syökäämme ja juokaamme, sillä huomenna me kuolemme."
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
Niin kuului minun korviini Herran Sebaotin ilmoitus: "Totisesti, ei tämä teidän syntinne tule sovitetuksi, ei kuolemaanne saakka, sanoo Herra, Herra Sebaot".
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Näin sanoo Herra, Herra Sebaot: Mene tuon huoneenhaltijan tykö, Sebnan tykö, joka on linnan päällikkönä.
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
"Mitä sinulla täällä on asiaa, ja keitä sinulla täällä on, kun tänne itsellesi haudan hakkautat, hakkautat hautasi korkeuteen, kallioon itsellesi asunnon koverrat?"
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Katso, Herra heittää sinua, mies, rajusti: hän kouraisee sinut kokoon,
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
kääräisee sinut keräksi ja paiskaa pallona menemään maahan, jossa on laajuutta joka suuntaan. Sinne sinä kuolet, ja sinne jäävät sinun kunniavaunusi, sinä herrasi huoneen häpeä.
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
Minä syöksen sinut pois paikastasi; hän kukistaa sinut asemastasi.
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
Mutta sinä päivänä minä kutsun palvelijani Eljakimin, Hilkian pojan,
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
ja puetan hänen yllensä sinun ihokkaasi, vyötän hänet sinun vyölläsi ja panen sinun valtasi hänen käteensä, niin että hän on oleva isänä Jerusalemin asukkaille ja Juudan suvulle.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
Ja minä panen Daavidin huoneen avaimen hänen olallensa; ja hän avaa, eikä kukaan sulje, ja hän sulkee, eikä kukaan avaa.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
Minä lyön hänet vaarnaksi vahvaan paikkaan, ja hän tulee kunniaistuimeksi isänsä suvulle.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
Hänen varaansa ripustautuu hänen isänsä suvun kaikki paljous, vesat ja versot, kaikki pienet astiat, maljat ja ruukut kaikki.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
Sinä päivänä, sanoo Herra Sebaot, pettää vahvaan paikkaan lyöty vaarna, se katkeaa ja putoaa, ja kuorma, joka oli sen varassa, särkyy. Sillä Herra on puhunut.

< Isaya 22 >