< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
The burden concerning the Valley of Vision. What aileth thee now, that thou art wholly gone up to the housetops,
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
Thou that art full of uproar, a tumultuous city, a joyous town? Thy slain are not slain with the sword, nor dead in battle.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
All thy rulers are fled together, without the bow they are bound; all that are found of thee are bound together, they are fled afar off.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
Therefore said I: 'Look away from me, I will weep bitterly; strain not to comfort me, for the destruction of the daughter of my people.'
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
For it is a day of trouble, and of trampling, and of perplexity, from the Lord, the GOD of hosts, in the Valley of Vision; Kir shouting, and Shoa at the mount.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
And Elam bore the quiver, with troops of men, even horsemen; and Kir uncovered the shield.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
And it came to pass, when thy choicest valleys were full of chariots, and the horsemen set themselves in array at the gate,
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
And the covering of Judah was laid bare, that thou didst look in that day to the armour in the house of the forest.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
And ye saw the breaches of the city of David, that they were many; and ye gathered together the waters of the lower pool.
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
And ye numbered the houses of Jerusalem, and ye broke down the houses to fortify the wall;
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
ye made also a basin between the two walls for the water of the old pool — but ye looked not unto Him that had done this, neither had ye respect unto Him that fashioned it long ago.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
And in that day did the Lord, the GOD of hosts, call to weeping, and to lamentation, and to baldness, and to girding with sackcloth;
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
And behold joy and gladness, slaying oxen and killing sheep, eating flesh and drinking wine — 'Let us eat and drink, for tomorrow we shall die!'
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
And the LORD of hosts revealed Himself in mine ears: Surely this iniquity shall not be expiated by you till ye die, saith the Lord, the GOD of hosts.
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Thus saith the Lord, the GOD of hosts: Go, get thee unto this steward, even unto Shebna, who is over the house:
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
What hast thou here, and whom hast thou here, that thou hast hewed thee out here a sepulchre, thou that hewest thee out a sepulchre on high, and gravest a habitation for thyself in the rock?
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Behold, the LORD will hurl thee up and down with a man's throw; yea, He will wind thee round and round;
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
He will violently roll and toss thee like a ball into a large country; there shalt thou die, and there shall be the chariots of thy glory, thou shame of the lord's house.
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
And I will thrust thee from thy post, and from thy station shalt thou be pulled down.
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
And it shall come to pass in that day, that I will call my servant Eliakim the son of Hilkiah;
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
And I will clothe him with thy robe, and bind him with thy girdle, and I will commit thy government into his hand; and he shall be a father to the inhabitants of Jerusalem, and to the house of Judah.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
And the key of the house of David will I lay upon his shoulder; and he shall open, and none shall shut; and he shall shut, and none shall open.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
And I will fasten him as a peg in a sure place; and he shall be for a throne of honour to his father's house.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
And they shall hang upon him all the glory of his father's house, the offspring and the issue, all vessels of small quantity, from the vessels of cups even to all the vessels of flagons.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
In that day, saith the LORD of hosts, shall the peg that was fastened in a sure place give way; and it shall be hewn down, and fall, and the burden that was upon it shall be cut off; for the LORD hath spoken it.

< Isaya 22 >