< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
A message about the Valley of Vision (Jerusalem). What's happening? Why has everyone gone up onto the rooftops?
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
There are shouts and commotion all over the city with people celebrating. Your dead weren't killed by the sword or in battle.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
All your leaders ran away together; they were captured without resistance. All your people trying to escape were captured together, even though they had run a long way away.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
That's why I said, “Go away! Let me mourn in peace. Don't insist on comforting me as the daughter of my people is ruined.”
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
For the Lord has a day of defeat, of panic and confusion in the Valley of Vision, a day of tearing down walls and crying for help to the mountains.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
The Elamites pick up their quivers full of arrows, and prepare their chariots and horsemen, while the people of Kir uncover their shields ready for battle.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
Your most productive valleys are now full of enemy chariots; and their cavalry are at your gates!
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
Judah's defenses have been stripped away and so at that time you went looking for weapons in the Palace of the Forest.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
You examined the breaks in the walls of the City of David and found there were many. You had water collect in the lower pool.
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
Your reviewed the number of houses in the city and demolished some to provide stone to repair the walls.
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
You built a reservoir inside the walls for the waters from the old pool, but you did not respect its Maker or think about the One who planned it long ago.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
At that time the Lord, the Lord Almighty, was calling you to weep and mourn, to shave your heads and wear sackcloth.
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
Instead, you go on happily partying! You slaughter cattle and sheep so you can have your feasts, eating meat and drinking wine, saying, “Let's eat and drink, because we're going to die tomorrow!”
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
The Lord Almighty has made this clear to me: “I will not forgive this sin till your dying day, says the Lord, the Lord Almighty.”
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
This is what the Lord, the Lord Almighty, told me to do. “Go to Shebna, the palace manager, and give him this message:
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
‘What are you doing here? Who do you think you are, cutting out a tomb for yourself high up on a hill, carving out for yourself a place to rest?
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Watch out, you “great man”! The Lord is about to grab you and violently toss you aside.
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
He's going to roll you up into a ball, and throw you far away into a vast country. You will die there, and that's where the chariots you were so proud of will remain. You're a disgrace to your lord's royal family.
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
I will push you out of office, I will strip you of your position.
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
After that I will call for my servant, Eliakim, son of Hilkiah.
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
I will put your robe and place your sash around him, and I will give your authority to him. He will be a father to the people living in Jerusalem and Judah.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
I will give him the key to the house of David. What he opens, nobody can shut; what he shuts, nobody can open.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
I will drive him like a nail hammered securely into a wall. He will bring honor to his family.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
The heavy burden of his father's family will hang on him—all the descendants and the inlaws—all the little containers, bowls and all kinds of jars.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
So the time will come, declares the Lord Almighty, when the nail will come out of the wall, even though it was hammered in securely. It will break off and fall down, and everything hanging on it will fall down too. The Lord has spoken.

< Isaya 22 >