< Isaya 22 >
1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
The burden of the valley of vision. What does it mean to you, then, that each of you have even climbed to the rooftops?
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
Filled with clamor, a busy city, an exultant city: your dead have not been slain by the sword, nor did they die in battle.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
All your leaders have fled together, and they have been bound by hardship. All who were found were chained together. They have fled far away.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
For this reason, I said: “Depart from me. I will weep bitterly. Make no attempt to console me, over the devastation of the daughter of my people.”
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
For it is a day of death, and of trampling, and of weeping to the Lord, the God of hosts, in the valley of vision: examining the wall and the magnificence above the mountain.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
And Elam took up the quiver and the chariot of the horseman; and he stripped the wall of the shield.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
And your elect valleys will be filled with chariots, and the horsemen will position themselves at the gates.
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
And the covering of Judah will be exposed, and in that day, you will see the weaponry of the forest house.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
And you will see breaches in the city of David, for these have been multiplied. But you have gathered together the waters of the lower fish-pool.
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
And you have numbered the houses of Jerusalem. And you have destroyed the houses in order to fortify the wall.
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
And you have made a pit between two walls for the waters of the ancient fish-pool. But you have not gazed upward to him who made it, and you have not considered, even from a distance, its Maker.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
And in that day, the Lord, the God of hosts, will call to weeping and mourning, to baldness and the wearing of sackcloth.
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
But behold: gladness and rejoicing, the killing of calves and the slaughter of rams, the eating of meat and the drinking of wine: “Let us eat and drink, for tomorrow we will die.”
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
And the voice of the Lord of hosts was revealed in my ears: “Surely this iniquity will not be forgiven you, until you die,” says the Lord, the God of hosts.
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Thus says the Lord, the God of hosts: Go forth and enter to him who lives in the tabernacle, to Shebna, who is in charge of the temple, and you shall say to him:
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
“What are you here, or who are you claiming to be here? For you have hewn a sepulcher for yourself here. You have diligently hewn a memorial in a rock, as a tabernacle to yourself.
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Behold, the Lord will cause you to be carried away, like a domesticated rooster, and he will remove you, like an outer garment.
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
He will crown you with a crown of tribulation. He will toss you like a ball into a broad and spacious land. There you will die, and there the chariot of your glory will be, for it is a shame to the house of your Lord.”
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
And I will expel you from your station, and I will depose you from your ministry.
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
And this shall be in that day: I will call my servant Eliakim, the son of Hilkiah.
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
And I will clothe him with your vestment, and I will strengthen him with your belt, and I will give your authority to his hand. And he shall be like a father to the inhabitants of Jerusalem and to the house of Judah.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
And I will place the key of the house of David upon his shoulder. And when he opens, no one will close. And when he closes, no one will open.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
And I will fasten him like a peg in a trustworthy place. And he will be upon a throne of glory in the house of his father.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
And they will suspend over him all the glory of his father’s house: various kinds of vessels and every little article, from the vessels of bowls even to every instrument of music.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
In that day, says the Lord of hosts, the peg which was fastened in a trustworthy place shall be taken away. And he will be broken, and he will fall, and he will perish, along with all that had depended upon him, because the Lord has spoken it.