< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
Profeti imod Synernes Dal. Hvad fattes dig dog, at du med alle dine saaledes stiger op paa Tagene?
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
Du, som var fuld af Brusen, du støjende Stad, du jublende By! dine ihjelslagne ere ikke ihjelslagne med Sværd og ikke døde i Krigen.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
Alle dine Fyrster ere flygtede til Hobe, tiden Bue ere de fangne; alle; som fandtes i dig, ere fangne, til Hobe, de maatte fly langt bort.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
Derfor siger jeg: Ser bort fra mig, jeg vil beskelig græde; trænger ikke paa for at trøste mig over mit Folks Datters Ødelæggelse.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
Thi der er en Forstyrrelses og Nedtrædelses og Forvirrings Dag fra Herren, den Herre Zebaoth, i Synernes Dal, paa Hvilken Murene blive nedbrudte, og man raaber imod Bjergene.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
Og Elam bar Kogger, fulgt af Vogne med Mænd paa og af Ryttere, og Kir blottede Skjoldet.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
Og det skete, at dine udvalgte Dale bleve fulde af Vogne, og Ryttere toge Stilling imod Porten.
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
Og han borttog Dækket fra Juda; og du saa dig om paa den Dag efter Rustningen i Skovhuset.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
Og I saa Revnerne paa Davids Stad, at de vare mange, og I samlede den nederste Dams Vand.
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
Og I talte Jerusalems-Huse og nedbrøde Huse for at befæste Muren.
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
Og I gjorde en Grav imellem de tvende Mure for Vandet af den gamle Dam; men I saa ikke hen til ham, som havde beskikket det, til ham, som havde besluttet det for lang Tid siden, saa I ikke.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
Og Herren, den Herre Zebaoth, opfordrede paa den Dag til Graad og Sorg og til at gøre Hovedet skaldet og til at ombinde sig med Sæk.
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
Men se, der er Fryd og Glæde, man ihjelslaar Øksne og slagter Faar, æder Kød og drikker Vin: „Lader os æde og drikke; thi vi skulle dø i Morgen!‟
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
Men den Herre Zebaoth har saaledes aabenbaret sig for mine Øren: Denne Misgerning skal ikke udsones for eder, inden I dø! siger Herren, den Herre Zebaoth.
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Saa sagde Herren, den Herre Zebaoth: Gak, kom ind til denne Rentemester, til Sebna, som er Hofmester, og sig til ham:
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
Hvad har du her? og hvem har du her, at du har hugget dig her en Grav? som den, der lader hugge sin Grav i det høje, som den, der lader sig en Bolig udhule i Klippen!
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Se, Herren skal bortkaste dig med et Kast, du Mand! og skjule dig aldeles.
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
Han skal sno dig sammen i en Snoning, som en Bold, hen til et vidt og bredt Land; der skal du dø, og der skulle dine herlige Vogne komme hen, du, som er en Skændsel for din Herres Hus!
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
Og jeg vil støde dig ned fra dit Stade, og han skal nedkaste dig fra din Plads,
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
Og det skal ske paa den Dag, da vil jeg kalde ad min Tjener Eliakim, Hilkias Søn.
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
Og jeg vil iføre ham din Kjortel og styrke ham med dit Bælte og give dit Herredømme i hans Haand; og han skal være en Fader for dem, som bo i Jerusalem, og for Judas Hus.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
Og jeg vil lægge Nøglen til Davids Hus paa hans Skuldre, og han skal oplade, og ingen skal tillukke, og han skal tillukke, og ingen skal oplade.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
Og jeg vil fæste ham som en Nagle paa et fast Sted, og han skal være et Ærens Sæde for sin Faders Hus.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
Og de skulle hænge paa ham al hans Faders Hus's Herlighed, de ædle og de vilde Skud, alle Smaakar, baade Bægere og alle Flasker.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
Paa den Dag, siger den Herre Zebaoth, skal Naglen borttages, den, som var fæstet paa et fast Sted, og den skal afhugges og falde, og den Byrde, som hang derpaa, skal ødelægges; thi Herren har talt det.

< Isaya 22 >