< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
Breme pustinji na moru. Kao vihori koji prolaze na jug, tako æe doæi iz pustinje, iz zemlje strašne.
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
Ljuta utvara javi mi se. Nevjernik nevjeru èini, pustošnik pustoši; hodi, Elame; opkoli, Midijo! svemu uzdisanju uèiniæu kraj.
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
Zato su bedra moja puna bola; muke me obuzeše kao kad se muèi porodilja; zgurih se èujuæi, prepadoh se videæi.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
Srce mi se smete, groza me poduze; noæ milina mojih pretvori mi se u strah.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
Postavi sto, stražar neka straži; jedi, pij; ustajte knezovi, mažite štitove.
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
Jer ovako mi reèe Gospod: idi, postavi stražara da ti javi što vidi.
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
I vidje kola, i dva reda konjika; kola s magarcima i kola s kamilama; i pažaše dobro velikom pažnjom.
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
I povika kao lav: gospodaru, ja stojim jednako na straži danju, i stojim na straži po svu noæ.
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
I evo doðoše na kolima ljudi, u dva reda konjici. Tada povika i reèe: pade, pade Vavilon, i svi rezani likovi bogova njegovijeh razbiše se o zemlju.
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
Vršaju moj, i pšenice gumna mojega! što èuh od Gospoda nad vojskama, Boga Izrailjeva, javih vam.
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
Breme Dumi. Vièe k meni neko sa Sira: stražaru! šta bi noæas? stražaru! šta bi noæas?
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
Stražar reèe: doæi æe jutro, ali i noæ; ako æete tražiti, tražite, vratite se, doðite.
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
Breme Arapskoj. Po šumama u Arapskoj noæivaæete, putnici Dedanski!
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
Iznesite vode pred žedne, koji živite u zemlji Temi, sretite s hljebom bjegunca.
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
Jer æe bježati od maèa, od maèa gologa, od luka zapetoga i od žestokoga boja.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
Jer ovako mi reèe Gospod: za godinu, kao što je godina najamnièka, nestaæe sve slave Kidarske.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
I što ostane hrabrijeh strijelaca sinova Kidarskih, biæe malo; jer Gospod Bog Izrailjev reèe.

< Isaya 21 >