< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
وحی درباره بیابان بحر: چنانکه گردباد در جنوب می‌آید، این نیز از بیابان از زمین هولناک می‌آید.۱
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
رویای سخت برای من منکشف شده است، خیانت پیشه خیانت می‌کند و تاراج کننده تاراج می‌نماید. ای عیلام برآی و‌ای مدیان محاصره نما. تمام ناله آن را ساکت گردانیدم.۲
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
از این جهت کمر من از شدت درد پر شده است و درد زه مثل درد زنی که می‌زاید مرادرگرفته است. پیچ و تاب می‌خورم که نمی توانم بشنوم، مدهوش می‌شوم که نمی توانم ببینم.۳
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
دل من می‌طپید و هیبت مرا ترسانید. او شب لذت مرابرایم به خوف مبدل ساخته است.۴
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
سفره را مهیاساخته و فرش را گسترانیده به اکل و شرب مشغول می‌باشند. ای سروران برخیزید و سپرهارا روغن بمالید.۵
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
زیرا خداوند به من چنین گفته است: «برو ودیده بان را قرار بده تا آنچه را که بیند اعلام نماید.۶
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
و چون فوج سواران جفت جفت و فوج الاغان وفوج شتران را بیند آنگاه به دقت تمام توجه بنماید.»۷
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
پس او مثل شیر صدا زد که «ای آقا من دائم در روز بر محرس ایستاده‌ام و تمامی شب بردیده بانگاه خود برقرار می‌باشم.۸
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
و اینک فوج مردان و سواران جفت جفت می‌آیند و او مزیدکرده، گفت: بابل افتاد افتاده است و تمامی تمثال های تراشیده خدایانش را بر زمین شکسته‌اند.»۹
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
‌ای کوفته شده من و‌ای محصول خرمن من آنچه از یهوه صبایوت خدای اسرائیل شنیدم به شما اعلام می‌نمایم.۱۰
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
وحی درباره دومه: کسی از سعیر به من ندا می‌کند که «ای دیده بان از شب چه خبر؟ ای دیده بان از شب چه خبر؟»۱۱
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
دیده بان می‌گوید که صبح می‌آید و شام نیز. اگر پرسیدن می‌خواهید بپرسید و بازگشت نموده، بیایید.»۱۲
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
وحی درباره عرب: ای قافله های ددانیان در جنگل عرب منزل کنید.۱۳
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
‌ای ساکنان زمین تیما تشنگان را به آب استقبال کنید و فراریان را به خوراک ایشان پذیره شوید.۱۴
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
زیرا که ایشان از شمشیرها فرارمی کنند. از شمشیر برهنه و کمان زه شده و ازسختی جنگ.۱۵
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
زانرو که خداوند به من گفته است بعد ازیکسال موافق سالهای مزدوران تمامی شوکت قیدار تلف خواهد شد.۱۶
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
و بقیه شماره تیراندازان و جباران بنی قیدار قلیل خواهد شدچونکه یهوه خدای اسرائیل این را گفته است.۱۷

< Isaya 21 >