< Isaya 21 >
1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
Spriedums par jūras tuksnesi. Tā kā aukas no dienvidiem(Negebas), kas visu apgāž, tā nāks no tuksneša, no briesmīgas zemes.
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
Grūta parādīšana man darīta zināma. Laupītājs laupa, postītājs posta. Nāc šurp, Elam, apstāj, Medija! Visām nopūtām par tiem es darīšu galu.
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
Tādēļ mani gurni dreb, raizes mani sagrābušas, kā dzemdētājas raizes. Es lokos, ka vairs nedzirdu, un iztrūcinājos, ka vairs neredzu.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
Mana sirds trīc, izbailes mani iztrūcina, mīļā nakts tumsa man palikusi par biedēkli.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
Sataisi galdu, nostādi vaktis, ēd, dzer! Ceļaties, virsnieki, svaidat bruņas.
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
Jo tā Tas Kungs uz mani sacījis: ej, nostādi vaktnieku, lai tas stāsta, ko redz.
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
Un viņš redzēja ratus, jātniekus pa pāriem, ēzeļu pulku, kamieļu pulku, un viņš klausīdamies klausījās it uzmanīgi,
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
Un sauca ar lauvas balsi: Kungs, es stāvu uz vakts torņa visu cauru dienu un vaktēdams vaktēju caurām naktīm.
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
Redzi, tur nāk rati ar vīriem un jātnieki pa pāriem. Tad viņš atbildēja un sacīja: kritusi, kritusi Bābele, un visi viņas dievekļu tēli ir sadauzīti pie zemes.
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
Ak tu mans izkultais, tu mana klona labībiņa! Ko es esmu dzirdējis no Tā Kunga Cebaot, Israēla Dieva, to jums esmu pasludinājis.
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
Spriedums par Dumu: uz mani sauc no Seīra: sargs, cik gara vēl nakts? Sargs, cik gara vēl nakts?
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
Tas sargs saka: rīts nāk un atkal nakts. Ja gribat vaicāt, vaicājiet! Atgriežaties, nāciet!
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
Spriedums par Arābiju: Arābijas tuksnešos paliekat par nakti, jūs Dedana ceļa vīri.
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
Nāciet izslāpušiem pretī ar ūdeni, jūs Temas zemes iedzīvotāji, pasniedziet maizi bēdzējiem.
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
Jo tie bēg no zobena, no izvilkta zobena un no uzvilkta stopa un no briesmīgas kaujas.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
Jo tā Tas Kungs uz mani sacījis: gada laikā, kādi ir algādža gadi, tad beigsies visa Ķedara godība.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
Un strēlnieku atlikums no tiem vareniem Ķedara bērniem būs mazums; jo Tas Kungs, Israēla Dievs, to ir runājis.