< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
Malheur accablant du désert de la mer. Comme des tourbillons viennent de l’Africus, il vient du désert, d’une terre affreuse.
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
Une vision pénible m’a été annoncée; celui qui est incrédule agit infidèlement; et celui qui dépeuple, dévaste. Monte, Elam; Mède, assiège; j’ai fait cesser tous ses gémissements.
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
À cause de cela mes reins sont remplis de douleur; l’angoisse s’est emparée de moi comme l’angoisse d’une femme en travail; je suis tombé, lorsque j’ai entendu; j’ai été tout troublé, lorsque j’ai vu.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
Mon cœur s’est flétri; des ténèbres m’ont frappé de stupeur; Babylone que je chérissais m’est devenue un sujet d’étonnement.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
Dresse la table; contemple dans une guérite ceux qui mangent et qui boivent: levez-vous, princes, saisissez le bouclier.
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
Car voici ce que m’a dit le Seigneur: Va, et place une sentinelle; et tout ce qu’elle aura vu, qu’elle l’annonce.
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
Et elle vit un chariot conduit par deux cavaliers, l’un qui montait un âne, et l’autre qui montait un chameau; et elle considéra soigneusement d’un œil très attentif.
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
Et elle cria comme un lion: Je suis dans la guérite du Seigneur, m’y tenant continuellement pendant le jour, et je fais ma garde, m’y tenant les nuits entières.
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
Voici que vient cet homme qui monte le chariot aux deux montures des cavaliers; et il répondit et dit: Elle est tombée, elle est tombée, Babylone, et toutes les images de ses dieux, taillées au ciseau, ont été brisées contre terre.
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
Mon battage, et vous, fils de mon aire, ce que j’ai ouï du Seigneur des armées. Dieu d’Israël, je vous l’ai annoncé.
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
Malheur accablant de Duma. Il me crie de Séir: Garde, qu’annonces-tu de la nuit? garde, qu’annonces-tu de la nuit?
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
Le garde dit: Le matin est venu, et la nuit; si vous cherchez, cherchez; convertissez-vous, venez.
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
Malheur accablant dans l’Arabie. Dans le bois, le soir, vous dormirez, dans les sentiers de Dédanim.
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
Venant au-devant de celui qui a soif, portez de l’eau, vous qui habitez la terre du midi, avec des pains venez au-devant de celui qui fuit.
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
Car à la face des glaives ils ont fui, à la face du glaive suspendu, à la face de l’arc bandé, à la face d’un grave combat:
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
Parce que voici ce que me dit le Seigneur: Encore une année comptée comme l’année d’un mercenaire, et toute gloire de Cédar sera enlevée.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
Et le reste du nombre des forts archers de Cédar seront diminués; car le Seigneur Dieu d’Israël a parlé.

< Isaya 21 >