< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
Oracle contre le désert de la mer. Comme l'ouragan du midi s'avance, ainsi il arrive du désert, de la terre redoutable.
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
Une vision menaçante m'a été révélée: le pillard pille et le dévastateur dévaste. « Avance, Elam! Assiège, Mède! A tous les soupirs je vais mettre un terme. »
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
C'est pourquoi mes reins sont remplis d'angoisses, des douleurs me saisissent pareilles aux douleurs de la femme en travail; le tourment m'ôte l'ouïe, et les angoisses la vue;
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
mon cœur s'égare; l'horreur m'assaille; de ma nuit de réjouissances on a fait une nuit de terreur.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
On dresse la table, la sentinelle veille, on mange, on boit: « Debout! chefs, oignez le bouclier! »
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
Car ainsi m'a parlé le Seigneur: Va, place la sentinelle: ce qu'elle verra, elle te le rapportera.
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
Elle vit de la cavalerie, des cavaliers sur des chevaux, deux à deux, des cavaliers sur des ânes, des cavaliers sur des chameaux, et elle écouta, écoutant avec grande attention.
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
Et elle cria comme un lion: Avec constance, Seigneur, je me tenais le jour dans la vedette et j'étais à mon poste toutes les nuits:
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
et voici venir de la cavalerie, des cavaliers sur des chevaux deux à deux. Puis reprenant la parole, elle dit: Babel tombe, tombe, et toutes ses idoles brisées jonchent la terre.
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
O toi, mon peuple qu'on triture, mon grain qui est sur l'aire! Ce que j'ai ouï de l'Éternel des armées, Dieu d'Israël, je vous l'ai déclaré.
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
Oracle contre Duma. De Séïr on me crie: Sentinelle, que reste-t-il de la nuit, que reste-t-il de la nuit?
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
La sentinelle dit: Le matin vient, puis aussi la nuit. Si vous voulez interroger, interrogez! Revenez-y!
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
Oracle contre l'Arabie. Dans les steppes d'Arabie vous passez la nuit, caravanes de Dedan!
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
Au-devant de ces hommes altérés viennent avec de l'eau les habitants du pays de Théma: ils présentent du pain aux fugitifs,
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
car ils fuient devant les épées, devant l'épée nue, et devant l'arc bandé, et devant le poids de la guerre.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
Car ainsi me parla le Seigneur: Encore une année, telle que les années du mercenaire, et c'en est fait de toute la gloire de Cédar.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
Et le nombre restant des vaillants archers des enfants de Cédar, sera petit, car l'Éternel, Dieu d'Israël, l'a prononcé.

< Isaya 21 >