< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
oracle wilderness sea like/as whirlwind in/on/with Negeb to/for to pass from wilderness to come (in): come from land: country/planet to fear
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
vision severe to tell to/for me [the] to act treacherously to act treacherously and [the] to ruin to ruin to ascend: rise Elam to confine Media all sighing her to cease
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
upon so to fill loin my anguish pang to grasp me like/as pang to beget to twist from to hear: hear to dismay from to see: see
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
to go astray heart my shuddering to terrify me [obj] twilight desire my to set: make to/for me to/for trembling
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
to arrange [the] table to overlay [the] rug to eat to drink to arise: rise [the] ruler to anoint shield
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
for thus to say to(wards) me Lord to go: went to stand: stand [the] to watch which to see: see to tell
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
and to see: see chariot pair horseman chariot donkey chariot camel and to listen attentiveness many attentiveness
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
and to call: call out lion upon lookout Lord I to stand: stand continually by day and upon charge my I to stand all [the] night
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
and behold this to come (in): come chariot man pair horseman and to answer and to say to fall: fall to fall: fall Babylon and all idol God her to break to/for land: soil
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
threshed my and son: type of threshing floor my which to hear: hear from with LORD Hosts God Israel to tell to/for you
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
oracle Dumah to(wards) me to call: call to from Seir to keep: guard what? from night to keep: guard what? from night
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
to say to keep: guard to come morning and also night if to enquire [emph?] to enquire to return: again to come
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
oracle in/on/with Arabia in/on/with wood in/on/with Arabia to lodge caravan Dedanite
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
to/for to encounter: meet thirsty to come water to dwell land: country/planet Tema in/on/with food: bread his to meet to wander
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
for from face: before sword to wander from face: before sword to leave and from face: before bow to tread and from face: before heaviness battle
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
for thus to say Lord to(wards) me in/on/with still year like/as year hired and to end: finish all glory Kedar
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
and remnant number bow mighty man son: descendant/people Kedar to diminish for LORD God Israel to speak: speak

< Isaya 21 >