< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
The prophecy concerning the desert of the sea. As storms which rush along through the south, So it cometh from the desert, From the terrible land.
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
A grievous vision was revealed to me; The plunderer plundereth, and the destroyer destroyeth. “Go up, O Elam! Besiege, O Media! All sighing do I make to cease.”
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
Therefore are my loins full of pain; Pangs have seized me, as the pangs of a woman in travail; For convulsions I cannot hear; For anguish I cannot see.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
My heart panteth, Terror hath seized upon me; The evening of my desire is changed into horror.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
The table is prepared; the watch is set; They eat; they drink; “Arise, ye princes! Anoint the shield!”
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
For thus said the Lord unto me: “Go, set a watchman, Who shall declare what he seeth.”
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
And he saw a troop, horsemen in pairs, Riders on asses, and riders on camels, And he watched with the utmost heed.
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
Then he cried like a lion: “My Lord, I stand continually upon the watch-tower in the daytime, And keep my post all the night;
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
And behold, there cometh a troop, Horsemen in pairs.” Again also he lifted up his voice, and said: “Fallen, fallen is Babylon, And all the graven images of her gods are cast broken to the ground.”
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
O my threshing, and the corn of my floor! What I have heard from Jehovah of hosts, the God of Israel, That have I declared to you.
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
The prophecy concerning Dumah. A voice came to me from Seir: “Watchman, what of the night? Watchman, what of the night?”
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
The watchman saith: “Morning cometh, and also night. If ye will inquire, inquire! Return, come!”
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
The prophecy against the Arabians. In the thickets of Arabia shall ye lodge, O ye caravans of Dedan!
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
The inhabitants of the land of Tema Bring water to the thirsty; They come to meet the fugitive with bread.
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
For they flee from swords, From the drawn sword, And from the bent bow, And from the fury of war.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
For thus saith the Lord to me: Within one year, according to the years of a hireling, Shall all the glory of Kedar be consumed.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
The remainder of the mighty bowmen of the sons of Kedar shall be diminished; For Jehovah, the God of Israel, hath said it.

< Isaya 21 >