< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
The burden of the wilderness of the sea. Like windstorms in the south for passing through, It has come from the wilderness, From a fearful land.
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
A hard vision has been declared to me, The treacherous dealer is dealing treacherously, And the destroyer is destroying. Go up, O Elam, besiege, O Media, I have caused all its sighing to cease.
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
Therefore my loins have been filled [with] great pain, Pangs have seized me as pangs of a travailing woman, I have been bent down by hearing, I have been troubled by seeing.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
My heart has wandered, trembling has terrified me, He has made the twilight of my desire a fear to me,
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
Arrange the table, watch in the watchtower, Eat, drink, rise, you heads, anoint the shield,
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
For thus said the Lord to me: “Go, station the watchman, Let him declare that which he sees.”
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
And he has seen a chariot—a couple of horsemen, The rider of a donkey, the rider of a camel, And he has given attention—He has increased attention!
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
And he cries, “A lion, my lord! I am continually standing on a watchtower by day, And I am stationed on my ward whole nights.
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
And behold, this, the chariot of a man is coming, A couple of horsemen.” And he answers and says: “Fallen, fallen has Babylon, And He has broken all the carved images of her gods to the earth.
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
O my threshing, and the son of my floor, That which I heard from YHWH of Hosts, God of Israel, I have declared to you!”
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
The burden of Dumah. [One] is calling to me from Seir, “Watchman, what of the night? Watchman, what of the night?”
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
The watchman has said, “Morning has come, and also night, If you inquire, inquire, return, come.”
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
The burden on Arabia. You lodge in a forest in Arabia, O caravans of Dedanim.
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
Inhabitants of the land of Tema Have brought water to meet the thirsty, With his bread they came before a fugitive.
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
For they fled from the face of destructions, From the face of an outstretched sword, And from the face of a trodden bow, And from the face of the grievousness of battle.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
For thus said the Lord to me: “Within a year, as years of a hired worker, All the glory of Kedar has been consumed.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
And the remnant of the number of bow-men, The mighty of the sons of Kedar, are few, For YHWH, God of Israel, has spoken!”

< Isaya 21 >