< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
THE VISION OF THE DESERT. As though a whirlwind should pass through the desert, coming from a desert, [even] from such a land,
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
[so] a fearful and a grievous vision was declared to me: he that is treacherous deals treacherously, the transgressor transgresses. The Elamites are upon me, and the ambassadors of the Persians come against me: now will I groan and comfort myself.
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
Therefore are my loins filled with feebleness, and pangs have seized me as a travailing woman: I dealt wrongfully that I might not hear; I hasted that I might not see.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
My heart wanders, and transgression overwhelms me; my soul is occupied with fear.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
Prepare the table, eat, drink: arise, you princes, and prepare [your] shields.
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
For thus said the Lord to me, Go and station a watchman for yourself, and declare whatever you shall see.
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
And I saw two mounted horsemen, and a rider on an ass, and a rider on a camel.
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
Listen with great attention, and call you Urias to the watch-tower: the Lord has spoken. I stood continually during the day, and I stood in the camp all night:
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
and, behold, he comes riding in a chariot and pair: and he answered and said, Babylon is fallen, is fallen; and all her images and her idols have been crushed to the ground.
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
Hear, you that are left, and you that are in pain, hear what things I have heard of the Lord of hosts [which] the God of Israel has declared to us. THE VISION OF IDUMEA.
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
Call to me out of Seir; guard you the bulwarks.
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
I watch in the morning and the night: if you would enquire, enquire, and dwell by me.
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
You may lodge in the forest in the evening, or in the way of Daedan.
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
You that dwell in the country of Thaeman, bring water to meet him that is thirsty;
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
meet the fugitives with bread, because of the multitude of the slain, and because of the multitude of them that lose their way, and because of the multitude of swords, and because of the multitude of bent bows, and because of the multitude of them that have fallen in war.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
For thus said the Lord to me, Yet a year, as the year of an hireling, [and] the glory of the sons of Kedar shall fail:
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
and the remnant of the strong bows of the sons of Kedar shall be small: for the Lord God of Israel has spoken [it].

< Isaya 21 >