< Isaya 21 >

1 Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
Profeti imod Havets Ørk. Ligesom Hvirvelvinde fare frem i Syden, saa kommer det fra Ørken, fra det forfærdelige Land.
2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
Mig er kundgjort et haardt Syn: Røveren røver, og Ødelæggeren ødelægger; drag op, Elam! træng paa Madaj! jeg har gjort, at hvert Suk hører op.
3 Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
Derfor ere mine Lænder fulde af Smerter, Veer have betaget mig ligesom Veer den fødende; jeg vrider mig, saa jeg ikke kan høre, jeg er forfærdet, saa at jeg ikke kan se.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
Mit Hjerte er forvildet, Gru har forfærdet mig, Tusmørket, som var min Lyst, er blevet mig til Rædsel.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
Man dækker Bord, Vagten vaager, man æder, man drikker; — „gører eder rede, I Fyrster! salver Skjoldet!”
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
Thi saa sagde Herren til mig: Gak, sæt en Vægter ud, lad ham kundgøre, hvad han ser.
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
Og ser han Vogne, Ryttere parvis, Vogne, dragne af Asener, Vogne, dragne af Kameler, da skal han give Agt, nøje Agt.
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
Og han raabte som en Løve: Herre! jeg staar stadig paa Vagt om Dagen, jeg staar paa min Vare hver Nat.
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
Og se! da kom der Vogne med Folk, Ryttere parvis; og han svarede og sagde: Babel er falden, den er falden, og man har kastet alle dens Gudebilleder knuste til Jorden!
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
Du, min tærskede, og du, som har været lagt paa min Lo! det, jeg hørte af den Herre Zebaoth, Israels Gud, kundgjorde jeg eder.
11 Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
Profeti imod Duma. Der raaber en til mig fra Seir: Vægter, hvordan skrider Natten? Vægter, hvordan skrider Natten?
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
Vægteren siger: Der kommer Morgen, men ogsaa Nat; ville I spørge, saa spørger! kommer igen en anden Gang.
13 Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
Profeti imod Arabien. I skulle blive Natten over i Skoven i Arabien, I rejsende Hobe af Dedaniter!
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
De komme den tørstige i Møde med Vand; Indbyggerne i Themas Land møde den flygtende med Brød.
15 Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
Thi de flyede for Sværd, for det dragne Sværd, for den spændte Bue og for den svare Krig.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
Thi saa sagde Herren til mig: Endnu inden et Aar, som en Daglønners Aar, da skal al Kedars Herlighed faa Ende.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.
Og Tallet af Buerne, som blive tilbage for de vældige af Kedars Børn, skal formindskes; thi Herren, Israels Gud, har talt det.

< Isaya 21 >