< Isaya 20 >
1 Katika mwaka ule ambao jemadari mkuu alitumwa na Mfalme Sargoni wa Ashuru, naye akaja mpaka Ashdodi, akaushambulia na kuuteka,
L'année où Tartan s'avança sur Asdod, envoyé par Sargon, roi d'Assyrie, et où il assiégea et prit Asdod,
2 wakati ule Bwana alisema kwa kinywa cha Isaya mwana wa Amozi. Akamwambia, “Vua nguo ya gunia kutoka mwilini mwako na viatu kutoka miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akatembea huku na huko uchi, bila viatu.
en ce temps-là l'Éternel parla par l'intermédiaire d'Ésaïe, fils d'Amots, et dit: Va, et détache le cilice de tes reins, et ôte tes souliers de tes pieds. Et il fit ainsi, et alla sans manteau et nu-pieds.
3 Kisha Bwana akasema, “Kama vile mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na bila viatu kwa miaka mitatu, kama ishara na dalili mbaya dhidi ya nchi ya Misri na Kushi,
Alors l'Éternel dit: De même que mon serviteur Ésaïe va sans manteau et nu-pieds, pendant trois ans signe et présage pour l'Egypte et pour l'Éthiopie,
4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawaongoza mateka wa Wamisri, na watu wa uhamisho wa Kushi, uchi na bila viatu, vijana hata wazee, wakiwa matako wazi, kwa aibu ya Wamisri.
de même le roi d'Assyrie emmènera les captifs de l'Egypte et les captifs de l'Ethiopie, jeunes hommes et vieillards, sans manteau et nu-pieds et le dos découvert, opprobre pour l'Egypte.
5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.
Alors ils seront consternés, et auront honte de l'Ethiopie qui avait leur confiance, et de l'Egypte dont ils se glorifiaient.
6 Katika siku ile watu wanaoishi katika pwani hii watasema, ‘Tazama lililowapata wale tuliowategemea, wale tuliowakimbilia kwa msaada na wokovu kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru! Tutawezaje basi kupona?’”
Et les habitants de cette côte diront en ce jour: Voilà où en sont ceux qui avaient notre confiance, vers qui nous fuyions, pour être secourus, pour être délivrés du roi d'Assyrie! et nous, comment pourrions-nous échapper?