< Isaya 20 >

1 Katika mwaka ule ambao jemadari mkuu alitumwa na Mfalme Sargoni wa Ashuru, naye akaja mpaka Ashdodi, akaushambulia na kuuteka,
L'année que Tanathan entra dans Azot, quand il y fut envoyé par Arna, roi des Assyriens, et qui assiégea la ville et s'en empara;
2 wakati ule Bwana alisema kwa kinywa cha Isaya mwana wa Amozi. Akamwambia, “Vua nguo ya gunia kutoka mwilini mwako na viatu kutoka miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akatembea huku na huko uchi, bila viatu.
Le Seigneur parla à Isaïe, fils d'Amos, disant: Pars, et ôte le cilice de tes reins; dénoue les sandales de tes pieds, et fais comme je te dis; voyage nu et déchaussé.
3 Kisha Bwana akasema, “Kama vile mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na bila viatu kwa miaka mitatu, kama ishara na dalili mbaya dhidi ya nchi ya Misri na Kushi,
Et le Seigneur dit: Comme mon serviteur Isaïe a voyagé trois ans nu et déchaussé, pour être pendant trois ans un sujet de signes et de prodiges pour les Éthiopiens et les Égyptiens;
4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawaongoza mateka wa Wamisri, na watu wa uhamisho wa Kushi, uchi na bila viatu, vijana hata wazee, wakiwa matako wazi, kwa aibu ya Wamisri.
Ainsi le roi des Assyriens emmènera une foule de captifs de l'Égypte et de l'Éthiopie, jeunes et vieux, nus, déchaussés, laissant à découvert la honte de l'Égypte.
5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.
Alors les Israélites rougiront à juste titre des Éthiopiens, en qui ils espéraient; car ils avaient mis leur gloire en eux.
6 Katika siku ile watu wanaoishi katika pwani hii watasema, ‘Tazama lililowapata wale tuliowategemea, wale tuliowakimbilia kwa msaada na wokovu kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru! Tutawezaje basi kupona?’”
Et en ce jour les habitants de cette terre diront: Voilà que nous avions cru trouver en eux un refuge et un secours, et ils n'ont pu se sauver du roi des Assyriens; comment nous sauverons-nous nous-mêmes?

< Isaya 20 >