< Isaya 20 >

1 Katika mwaka ule ambao jemadari mkuu alitumwa na Mfalme Sargoni wa Ashuru, naye akaja mpaka Ashdodi, akaushambulia na kuuteka,
In the year of the coming in of Tartan to Ashdod, when Sargon king of Asshur sendeth him, and he fighteth against Ashdod, and captureth it,
2 wakati ule Bwana alisema kwa kinywa cha Isaya mwana wa Amozi. Akamwambia, “Vua nguo ya gunia kutoka mwilini mwako na viatu kutoka miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akatembea huku na huko uchi, bila viatu.
at that time spake Jehovah by the hand of Isaiah son of Amoz, saying, 'Go, and thou hast loosed the sackcloth from off thy loins, and thy sandal thou dost draw from off thy foot,' and he doth so, going naked and barefoot.
3 Kisha Bwana akasema, “Kama vile mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na bila viatu kwa miaka mitatu, kama ishara na dalili mbaya dhidi ya nchi ya Misri na Kushi,
And Jehovah saith, 'As My servant Isaiah hath gone naked and barefoot three years, a sign and a wonder for Egypt and for Cush,
4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawaongoza mateka wa Wamisri, na watu wa uhamisho wa Kushi, uchi na bila viatu, vijana hata wazee, wakiwa matako wazi, kwa aibu ya Wamisri.
so doth the king of Asshur lead the captivity of Egypt, and the removal of Cush, young and old, naked and barefoot, with seat uncovered — the nakedness of Egypt;
5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.
and they have been affrighted and ashamed of Cush their confidence, and of Egypt their beauty,
6 Katika siku ile watu wanaoishi katika pwani hii watasema, ‘Tazama lililowapata wale tuliowategemea, wale tuliowakimbilia kwa msaada na wokovu kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru! Tutawezaje basi kupona?’”
and the inhabitant of this isle hath said in that day — Lo, thus [is] our trust, Whither we have fled for help, To be delivered from the king of Asshur, And how do we escape — we?'

< Isaya 20 >