< Isaya 20 >
1 Katika mwaka ule ambao jemadari mkuu alitumwa na Mfalme Sargoni wa Ashuru, naye akaja mpaka Ashdodi, akaushambulia na kuuteka,
In the year in which Tartan, being sent by Sargon, the king of Assyria, came to Ashdod, and fought against Ashdod, and took it,
2 wakati ule Bwana alisema kwa kinywa cha Isaya mwana wa Amozi. Akamwambia, “Vua nguo ya gunia kutoka mwilini mwako na viatu kutoka miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akatembea huku na huko uchi, bila viatu.
at that time spake Jehovah through Isaiah the son of Amoz in this manner: Go, and loose the sackcloth from thy loins, and put off thy shoes from thy feet. And he did so, walking naked and barefoot.
3 Kisha Bwana akasema, “Kama vile mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na bila viatu kwa miaka mitatu, kama ishara na dalili mbaya dhidi ya nchi ya Misri na Kushi,
And Jehovah said: As my servant Isaiah hath walked naked and barefoot three years, a sign and a token for Egypt and Ethiopia,
4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawaongoza mateka wa Wamisri, na watu wa uhamisho wa Kushi, uchi na bila viatu, vijana hata wazee, wakiwa matako wazi, kwa aibu ya Wamisri.
so shall the king of Assyria lead the captives of Egypt, and prisoners of Ethiopia, young and old, naked and barefoot, with their hind parts uncovered, to the shame of the Egyptians.
5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.
Then shall they be afraid and ashamed on account of Ethiopia their trust, and of Egypt their glory.
6 Katika siku ile watu wanaoishi katika pwani hii watasema, ‘Tazama lililowapata wale tuliowategemea, wale tuliowakimbilia kwa msaada na wokovu kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru! Tutawezaje basi kupona?’”
The inhabitant of this coast shall say in that day, “Behold, so is it with them in whom we trusted, and to whom we fled for help, that we might be delivered from the king of Assyria. How then shall we escape?”