< Isaya 20 >

1 Katika mwaka ule ambao jemadari mkuu alitumwa na Mfalme Sargoni wa Ashuru, naye akaja mpaka Ashdodi, akaushambulia na kuuteka,
亞述王撒爾貢派遣總司令來到阿市多得,進攻克服阿市多得的那一年──
2 wakati ule Bwana alisema kwa kinywa cha Isaya mwana wa Amozi. Akamwambia, “Vua nguo ya gunia kutoka mwilini mwako na viatu kutoka miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akatembea huku na huko uchi, bila viatu.
那時上主曾藉阿摩茲的兒子依撒意亞發言說:「去!脫下你腰間的苦衣,除去你腳上的鞋! 」他就這樣作了,裸體赤足而行──
3 Kisha Bwana akasema, “Kama vile mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na bila viatu kwa miaka mitatu, kama ishara na dalili mbaya dhidi ya nchi ya Misri na Kushi,
上主說:「就如我的僕人依撒意亞,三年之久,裸體赤足而行,為埃及和雇士是一個預言和先兆;
4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawaongoza mateka wa Wamisri, na watu wa uhamisho wa Kushi, uchi na bila viatu, vijana hata wazee, wakiwa matako wazi, kwa aibu ya Wamisri.
同樣亞述王要將埃及的俘虜和雇士的流徙帶走,無論老幼,一律裸體赤足,露著下體,好羞辱埃及。」
5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.
人們將對他們的仰望雇士,對他們的光榮埃及,感到失望和羞慚。
6 Katika siku ile watu wanaoishi katika pwani hii watasema, ‘Tazama lililowapata wale tuliowategemea, wale tuliowakimbilia kwa msaada na wokovu kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru! Tutawezaje basi kupona?’”
這一帶海濱的居民,在那天要說:「看!這原是我們所依賴,跑去求救,藉以擺脫亞述王的人!我們又怎能逃避呢﹖」

< Isaya 20 >