< Isaya 2 >

1 Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:
This is what Isaiah the son of Amoz saw concerning Judah and Jerusalem.
2 Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote, utainuliwa juu ya vilima, na mataifa yote yatamiminika huko.
It shall happen in the latter days, that the mountain of the LORD's house shall be established on the top of the mountains, and shall be raised above the hills; and all nations shall flow to it.
3 Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
And many peoples shall come and say, "Come, let's go up to the mountain of the LORD, and to the house of the God of Jacob; and he will teach us of his ways, and we will walk in his paths." For out of Zion the law shall go forth, and the word of the LORD from Jerusalem.
4 Atahukumu kati ya mataifa na ataamua migogoro ya mataifa mengi. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
He will judge between the nations, and will decide concerning many peoples; and they shall beat their swords into plowshares, and their spears into pruning hooks. Nation shall not lift up sword against nation, neither shall they learn war any more.
5 Njooni, enyi nyumba ya Yakobo, tutembeeni katika nuru ya Bwana.
House of Jacob, come, and let us walk in the light of the LORD.
6 Umewatelekeza watu wako, nyumba ya Yakobo. Wamejaa ushirikina utokao Mashariki, wanapiga ramli kama Wafilisti na wanashikana mikono na wapagani.
For you have forsaken your people, the house of Jacob, because they are filled from the east, with those who practice divination like the Philistines, and they clasp hands with the children of foreigners.
7 Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao.
Their land is full of silver and gold, neither is there any end of their treasures. Their land also is full of horses, neither is there any end of their chariots.
8 Nchi yao imejaa sanamu, wanasujudia kazi za mikono yao, vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.
Their land also is full of idols. They worship the work of their own hands, that which their own fingers have made.
9 Kwa hiyo mwanadamu atashushwa na binadamu atanyenyekezwa: usiwasamehe.
So people bow down, people are low, therefore do not lift them up.
10 Ingieni kwenye miamba, jificheni ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake!
Enter into the rock, and hide in the dust, from before the terror of the LORD, and from the glory of his majesty.
11 Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa na kiburi cha wanadamu kitashushwa, Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.
The proud looks of humankind will be brought low, and the arrogance of people will be brought down; and the LORD alone will be exalted in that day.
12 Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi, kwa wote wanaojikweza (nao watanyenyekezwa),
For there will be a day of the LORD of hosts for all that is proud and haughty, and for all that is lifted up and high; and it shall be brought low:
13 kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana, na mialoni yote ya Bashani,
For all the cedars of Lebanon, that are high and lifted up, for all the oaks of Bashan,
14 kwa milima yote mirefu na vilima vyote vilivyoinuka,
For all the high mountains, for all the hills that are lifted up,
15 kwa kila mnara ulio mrefu sana na kila ukuta wenye ngome,
For every lofty tower, for every fortified wall,
16 kwa kila meli ya biashara, na kila chombo cha baharini cha fahari.
For all the ships of Tarshish, and for all pleasant imagery.
17 Majivuno ya mwanadamu yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa, Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,
The loftiness of man shall be bowed down, and the haughtiness of men shall be brought low; and the LORD alone shall be exalted in that day.
18 nazo sanamu zitatoweka kabisa.
The idols shall utterly pass away.
19 Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba, na kwenye mahandaki ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
Men shall go into the caves of the rocks, and into the holes of the earth, from before the terror of the LORD, and from the glory of his majesty, when he arises to shake the earth mightily.
20 Siku ile, watu watawatupia panya na popo sanamu zao za fedha na za dhahabu, walizozitengeneza ili waziabudu.
In that day, people will cast away their idols of silver and their idols of gold to the rodents and to the bats, which have been made for themselves to worship;
21 Watakimbilia kwenye mapango miambani na kwenye nyufa za miamba kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
to go into the caverns of the rocks, and into the clefts of the ragged rocks, from before the terror of the LORD, and from the glory of his majesty, when he arises to shake the earth mightily.
22 Acheni kumtumainia mwanadamu, ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake. Yeye ana thamani gani?
Stop trusting in man, whose breath is in his nostrils; for of what account is he?

< Isaya 2 >