< Isaya 2 >

1 Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:
The word that Isaias the son of Amos saw, concerning Juda and Jerusalem.
2 Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote, utainuliwa juu ya vilima, na mataifa yote yatamiminika huko.
And in the last days the mountain of the house of the Lord shall be prepared on the top of mountains, and it shall be exalted above the hills, and all nations shall flow unto it.
3 Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
And many people shall go, and say: Come and let us go up to the mountain of the Lord, and to the house of the God of Jacob, and he will teach us his ways, and we will walk in his paths: for the law shall come forth from Sion, and the word of the Lord from Jerusalem.
4 Atahukumu kati ya mataifa na ataamua migogoro ya mataifa mengi. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
And he shall judge the Gentiles, and rebuke many people: and they shall turn their swords into ploughshares, and their spears into sickles: nation shall not lift up sword against nation, neither shall they be exercised any more to war.
5 Njooni, enyi nyumba ya Yakobo, tutembeeni katika nuru ya Bwana.
O house of Jacob, come ye, and let us walk in the light of the Lord.
6 Umewatelekeza watu wako, nyumba ya Yakobo. Wamejaa ushirikina utokao Mashariki, wanapiga ramli kama Wafilisti na wanashikana mikono na wapagani.
For thou hast cast off thy people, the house of Jacob: because they are filled as in times past, and have had soothsayers as the Philistines, and have adhered to strange children.
7 Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao.
Their land is filled with silver and gold: and there is no end of their treasures.
8 Nchi yao imejaa sanamu, wanasujudia kazi za mikono yao, vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.
And their land is filled with horses: and their chariots are innumerable. Their land also is full of idols: they have adored the work of their own hands, which their own fingers have made.
9 Kwa hiyo mwanadamu atashushwa na binadamu atanyenyekezwa: usiwasamehe.
And man hath bowed himself down, and man hath been debased: therefore forgive them not.
10 Ingieni kwenye miamba, jificheni ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake!
Enter thou into the rock, and hide thee in the pit from the face of the fear of the Lord, and from the glory of his majesty.
11 Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa na kiburi cha wanadamu kitashushwa, Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.
The lofty eyes of man are humbled, and the haughtiness of men shall be made to stoop: and the Lord alone shall be exalted in that day.
12 Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi, kwa wote wanaojikweza (nao watanyenyekezwa),
Because the day of the Lord of hosts shall be upon every one that is proud and highminded, and upon every one that is arrogant, and he shall be humbled.
13 kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana, na mialoni yote ya Bashani,
And upon all the tall and lofty cedars of Libanus, and upon all the oaks of Basan.
14 kwa milima yote mirefu na vilima vyote vilivyoinuka,
And upon all the high mountains, and upon all the elevated hills.
15 kwa kila mnara ulio mrefu sana na kila ukuta wenye ngome,
And upon every high tower, and every fenced wall.
16 kwa kila meli ya biashara, na kila chombo cha baharini cha fahari.
And upon all the ships of Tharsis, and upon all that is fair to behold.
17 Majivuno ya mwanadamu yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa, Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,
And the loftiness of men shall be bowed down, and the haughtiness of men shall be humbled, and the Lord alone shall be exalted in that day.
18 nazo sanamu zitatoweka kabisa.
And idols shall be utterly destroyed.
19 Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba, na kwenye mahandaki ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
And they shall go into the holes of rocks, and into the caves of the earth from the face of the fear of the Lord, and from the glory of his majesty, when he shall rise up to strike the earth.
20 Siku ile, watu watawatupia panya na popo sanamu zao za fedha na za dhahabu, walizozitengeneza ili waziabudu.
In that day a man shall cast away his idols of silver, and his idols of gold, which he had made for himself to adore, moles and bats.
21 Watakimbilia kwenye mapango miambani na kwenye nyufa za miamba kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
And he shall go into the clefts of rocks, and into the holes of stones from the face of the fear of the Lord, and from the glory of his majesty, when he shall rise up to strike the earth.
22 Acheni kumtumainia mwanadamu, ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake. Yeye ana thamani gani?
Cease ye therefore from the man, whose breath is in his nostrils, for he is reputed high.

< Isaya 2 >