< Isaya 18 >

1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa, kando ya mito ya Kushi,
در آن سوی رودخانه‌های حبشه سرزمینی هست که قایقهای بادبانی در آبهایش رفت و آمد می‌کنند.
2 iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari kwa mashua za mafunjo juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi, kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.
سرزمینی که سفیران خود را بر قایقهایی ساخته شده از نی، به رود نیل می‌فرستد. ای سفیران تندرو به آن سرزمینی بروید که بین رودخانه‌ها است و قومی بلند بالا و نیرومند در آن زندگی می‌کنند قومی که همه جا خوف و هراس ایجاد کرده‌اند.
3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu, ninyi mnaoishi duniani wakati bendera itakapoinuliwa milimani, mtaiona, nayo tarumbeta itakapolia, mtaisikia.
ای مردم دنیا توجه کنید! به پرچمی که بر قلهٔ کوهها برافراشته می‌شود بنگرید و به صدای شیپوری که برای جنگ نواخته می‌شود گوش دهید!
4 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nitatulia kimya na kutazama kutoka maskani yangu, kama joto linalometameta katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la wakati wa mavuno.”
خداوند به من چنین فرموده است: «من از مکان خود به آرامی نظر خواهم کرد، به آرامی یک روز باصفای تابستانی و یک صبح دلپذیر پائیزی در وقت حصاد.»
5 Kwa maana, kabla ya mavuno, wakati wa kuchanua ukishapita na maua yakawa zabibu zinazoiva, atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi, naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.
زیرا پیش از این که حصاد را جمع کنند، درست پس از ریخته شدن شکوفه‌ها و رسیدن انگور، حبشه مانند درخت انگوری که شاخه‌هایش را با اره بریده باشند، نابود خواهد شد.
6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani na wanyama pori, ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi, nao wanyama pori wakati wote wa masika.
سربازان حبش در صحرا خواهند مرد و اجسادشان برای پرندگان شکاری و حیوانات وحشی واگذاشته خواهد شد. پرندگان شکاری در تابستان، و حیوانات وحشی در زمستان، از لاشه‌های آنها تغذیه خواهند کرد.
7 Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito, matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
اما زمانی خواهد رسید که این قوم قدبلند و نیرومند که همه جا خوف و هراس ایجاد می‌کردند و سرزمینشان میان رودخانه‌ها بود به اورشلیم که خداوند لشکرهای آسمان نام خود را در آن قرار داده است خواهند آمد و برای او هدیه خواهند آورد.

< Isaya 18 >