< Isaya 18 >
1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa, kando ya mito ya Kushi,
Malheur à la terre qui retentit par la cymbale de ses ailes, qui est au-delà des fleuves d’Ethiopie,
2 iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari kwa mashua za mafunjo juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi, kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.
Qui envoie des ambassadeurs sur la mer et sur des vaisseaux de papyrus. Allez, anges rapides, vers une nation arrachée et déchirée, vers un peuple terrible, après lequel il n’en est pas d’autre aussi terrible; vers une nation qui attend et qui est foulée aux pieds, dont les fleuves ont ravagé la terre.
3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu, ninyi mnaoishi duniani wakati bendera itakapoinuliwa milimani, mtaiona, nayo tarumbeta itakapolia, mtaisikia.
Vous tous habitants de l’univers, qui demeurez sur la terre, lorsque l’étendard sera élevé sur les montagnes, vous le verrez, et vous entendrez le bruit éclatant de la trompette;
4 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nitatulia kimya na kutazama kutoka maskani yangu, kama joto linalometameta katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la wakati wa mavuno.”
Parce que voici ce que le Seigneur me dit: Je me tiendrai en repos, et je considérerai en mon lieu comme la lumière de midi qui est claire, et comme un nuage de rosée au jour de la moisson.
5 Kwa maana, kabla ya mavuno, wakati wa kuchanua ukishapita na maua yakawa zabibu zinazoiva, atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi, naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.
Car avant la moisson il a fleuri tout entier, et son germe le plus avancé ne mûrira pas, et ses petites branches seront coupées avec les faux, et ce qui aura été laissé sera retranché ou rejeté.
6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani na wanyama pori, ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi, nao wanyama pori wakati wote wa masika.
Il sera en même temps abandonné aux oiseaux des montagnes et aux bêtes de la terre; et pendant tout l’été y seront les oiseaux, et toutes les bêtes de la terre y passeront l’hiver.
7 Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito, matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
En ce temps-là sera offert un présent au Seigneur des armées, par un peuple arraché et déchiré, par un peuple terrible, après lequel il n’en fut pas d’autre aussi terrible; par une nation qui attend, qui attend, et qui est foulée aux pieds, dont les fleuves ont ravagé la terre; offert dans le lieu du nom du Seigneur des armées, la montagne de Sion.