< Isaya 18 >

1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa, kando ya mito ya Kushi,
Wo to the lond, the cymbal of wyngis, which is biyende the flood of Ethiopie; that sendith messangeris bi the see,
2 iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari kwa mashua za mafunjo juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi, kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.
and in vessels of papirus on watris. Go, ye messangeris, to the folk drawun up and to-rent; to a ferdful puple, aftir which is noon other; to the folk abidynge and defoulid, whos lond the flodis han rauyschid; to the hil of the name of the Lord of oostis, to the hil of Sion.
3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu, ninyi mnaoishi duniani wakati bendera itakapoinuliwa milimani, mtaiona, nayo tarumbeta itakapolia, mtaisikia.
Alle ye dwelleris of the world, that dwellen in the lond, schulen se whanne a signe schal be reisid in the hillis, and ye schulen here the cry of a trumpe.
4 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nitatulia kimya na kutazama kutoka maskani yangu, kama joto linalometameta katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la wakati wa mavuno.”
For whi the Lord seith these thingis to me, Y schal reste, and Y schal biholde in my place, as the myddai liyt is cleer, and as a cloude of dew in the dai of heruest.
5 Kwa maana, kabla ya mavuno, wakati wa kuchanua ukishapita na maua yakawa zabibu zinazoiva, atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi, naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.
For whi al flouride out bifore heruest, aud vnripe perfeccioun buriownede; and the litle braunchis therof schulen be kit doun with sithis, and tho that ben left, schulen be kit awei. Thei schulen be schakun out,
6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani na wanyama pori, ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi, nao wanyama pori wakati wote wa masika.
and schulen be left togidere to the briddis of hillis, and to the beestis of erthe; and briddis schulen be on hym by a somer euerlastinge, and alle the beestis of erthe schulen dwelle bi wyntir on hym.
7 Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito, matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
In that tyme a yifte schal be brouyt to the Lord of oostis, of the puple drawun up and to-rent; of the puple ferdful, aftir which was noon other; of the folk abidynge and defoulid, whos lond floodis rauyschiden; the yifte schal be brouyt to the place of the name of the Lord of oostis, to the hil of Sion.

< Isaya 18 >