< Isaya 18 >
1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa, kando ya mito ya Kushi,
Oh, the lande shadowing with winges, which is beyond the riuers of Ethiopia,
2 iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari kwa mashua za mafunjo juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi, kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.
Sending ambassadours by the Sea, euen in vessels of reedes vpon the waters, saying, Go, ye swift messengers, to a nation that is scattered abroade, and spoyled, vnto a terrible people from their beginning euen hitherto: a nation by litle and litle, euen troden vnder foote, whose land the floods haue spoyled.
3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu, ninyi mnaoishi duniani wakati bendera itakapoinuliwa milimani, mtaiona, nayo tarumbeta itakapolia, mtaisikia.
Al ye the inhabitants of ye world and dwellers in the earth, shall see when he setteth vp a signe in the mountaines, and when he bloweth the trumpet, ye shall heare.
4 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nitatulia kimya na kutazama kutoka maskani yangu, kama joto linalometameta katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la wakati wa mavuno.”
For so the Lord saide vnto me, I will rest and beholde in my tabernacle, as the heate drying vp the rayne, and as a cloude of dewe in the heate of haruest.
5 Kwa maana, kabla ya mavuno, wakati wa kuchanua ukishapita na maua yakawa zabibu zinazoiva, atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi, naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.
For afore the haruest when the floure is finished, and the fruite is riping in the floure, then he shall cut downe the branches with hookes, and shall take away, and cut off the boughes:
6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani na wanyama pori, ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi, nao wanyama pori wakati wote wa masika.
They shall be left together vnto the foules of the mountaines, and to the beastes of the earth: for the foule shall sommer vpon it, and euery beast of the earth shall winter vpon it.
7 Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito, matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
At that time shall a present be brought vnto the Lord of hostes, (a people that is scattered abroade, and spoyled, and of a terrible people from their beginning hitherto, a nation, by litle and litle euen troden vnder foote, whose land the riuers haue spoyled) to the place of the Name of the Lord of hostes, euen the mount Zion.