< Isaya 17 >

1 Neno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
Malheur accablant de Damas. Voilà que Damas cessera d’être une cité, et elle sera un monceau de pierres en ruines.
2 Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
Les cités d’Aroër seront abandonnées aux troupeaux, et ils s’y reposeront, et il n’y aura personne qui les effrayera.
3 Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Et le soutien manquera à Ephraïm et le règne à Damas; et les restes de la Syrie seront comme la gloire des fils d’Israël,
4 “Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
Et il arrivera en ce jour-là que la gloire de Jacob sera atténuée, et que la graisse de sa chair se desséchera.
5 Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
Et il sera comme celui qui ramasse dans la moisson ce qui est resté, et son bras recueillera des épis; et il sera comme celui qui cherche des épis dans la vallée de Raphaïm.
6 Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yazaayo sana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.
Et il y sera laissé seulement comme une grappe de raisin, et comme, lorsqu’on secoue un olivier, son fruit restant sera de deux ou trois olives au sommet d’une branche, ou bien de quatre ou de cinq à ses cimes, dit le Seigneur Dieu d’Israël.
7 Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
En ce jour-là l’homme s’inclinera vers son Créateur, et ses yeux regarderont du côté du saint d’Israël.
8 Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
Et il ne s’inclinera pas du côté des autels qu’ont faits ses mains; et ce qu’ont façonné ses doigts, les bois sacrés et les temples, il ne les regardera pas.
9 Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
En ce jour-là, ses cités les plus fortes seront abandonnées comme les charrues et les moissons qui furent abandonnées à la vue des fils d’Israël; et tu seras déserte.
10 Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
Parce que tu as oublié le Dieu ton sauveur, et que de ton puissant secours tu ne t’es pas souvenue; c’est pour cela que tu planteras du bon plant, et que tu sèmeras une semence étrangère.
11 hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
Au jour de ta plantation c’était une vigne sauvage, et dès le matin ta semence fleurira; la moisson a été enlevée au jour de l’héritage, et tu en éprouveras une douleur grave.
12 Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi, wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Lo! Makelele ya mataifa wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
Malheur à la multitude de peuples nombreux; elle est comme la multitude des flots d’une mer mugissante; et le tumulte des troupes, comme le bruit des grandes eaux.
13 Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.
Des peuples feront un bruit, comme le bruit des eaux qui débordent, et il le menacera, et il fuira au loin; et il sera emporté comme la poussière des montagnes à la face du vent, et comme un tourbillon devant la tempête.
14 Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.
Il sera au temps du soir, et voici le trouble, au temps du matin, et il n’existera plus, voilà la part de ceux qui nous ont dévastés, et le sort de ceux qui nous ont pillés.

< Isaya 17 >