< Isaya 17 >
1 Neno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
The birthun of Damask. Lo! Damask schal faile to be a citee, and it schal be as an heep of stoonys in fallyng.
2 Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
The forsakun citees of Aroer schulen be to flockis; and tho schulen reste there, and noon schal be that schal make aferd.
3 Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And help schal ceesse fro Effraym, and a rewme fro Damask; and the relifs of Sirie schulen be as the glorie of the sones of Israel, seith the Lord of oostis.
4 “Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
And it schal be, in that dai the glorie of Jacob schal be maad thinne, and the fatnesse of his fleisch shal fade.
5 Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
And it schal be as gaderyng togidere that that is left in heruest, and his arm schal gadere eeris of corn, and it schal be as sekynge eeris of corn in the valei of Raphaym.
6 Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yazaayo sana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.
And there schal be left in it as a rasyn, and as the schakyng doun of the fruyt of olyue tre, as of tweyne ether of thre olyue trees in the hiynesse of a braunche, ether of foure ether of fyue; in the cooppis therof schal be the fruyt therof, seith the Lord God of Israel.
7 Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
In that dai a man schal be bowid to his maker, and hise iyen schulen biholde to the hooli of Israel.
8 Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
And he schal not be bowid to the auteris, whiche hise hondis maden, and whiche hise fyngris wrouyten; he schal not biholde wodis, and templis of idols.
9 Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
In that dai the citees of strengthe therof schulen be forsakun as plowis, and cornes that weren forsakun of the face of the sones of Israel; and thou schalt be forsakun.
10 Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
For thou hast foryete God, thi sauyour, and haddist not mynde on thi stronge helpere; therfor thou schalt plaunte a feithful plauntyng, and thou schalt sowe an alien seed.
11 hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
In the dai of thi plauntyng schal be a wielde vyne, and erli thi seed schal floure; ripe corne is takun awei in the dai of eritage, and Israel schal make sorewe greuousli.
12 Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi, wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Lo! Makelele ya mataifa wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
Wo to the multitude of many puplis, as the multitude of the see sownynge, and the noise of cumpenyes as the sown of many watris.
13 Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.
Puplis schulen sowne as the sown of flowynge watris, and God schal blame hym; and he schal fle fer, and he schal be rauyschid as the dust of hillis fro the face of the wynd, and as a whirlewynd bifor tempest.
14 Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.
In the time of euentide, and lo! disturbling; in the morewtid, and he schal not abide. This is the part of hem that destrieden vs, and the part of hem that rauyschiden vs.