< Isaya 17 >
1 Neno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
oracle Damascus behold Damascus to turn aside: depart from city and to be heap ruin
2 Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
to leave: forsake city Aroer to/for flock to be and to stretch and nothing to tremble
3 Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
and to cease fortification from Ephraim and kingdom from Damascus and remnant Syria like/as glory son: descendant/people Israel to be utterance LORD Hosts
4 “Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
and to be in/on/with day [the] he/she/it to languish glory Jacob and fatness flesh his to starve
5 Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
and to be like/as to gather harvest standing grain and arm his ear to reap and to be like/as to gather ear in/on/with Valley (of Rephaim) (Valley of) Rephaim
6 Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yazaayo sana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.
and to remain in/on/with him gleaning like/as shaking olive two three berry in/on/with head: top top four five in/on/with cleft her be fruitful utterance LORD God Israel
7 Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
in/on/with day [the] he/she/it to gaze [the] man upon to make him and eye his to(wards) holy Israel to see: see
8 Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
and not to gaze to(wards) [the] altar deed: work hand his and which to make finger his not to see: see and [the] Asherah and [the] pillar
9 Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
in/on/with day [the] he/she/it to be city security his like/as to leave: forsake [the] wood and [the] top which to leave: forsake from face: because son: descendant/people Israel and to be devastation
10 Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
for to forget God salvation your and rock security your not to remember upon so to plant plantation pleasantness and branch be a stranger to sow him
11 hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
in/on/with day plantation your to grow and in/on/with morning seed your to sprout heap harvest in/on/with day be weak: grieved and pain be incurable
12 Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi, wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Lo! Makelele ya mataifa wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
woe! crowd people many like/as to roar sea to roar [emph?] and roar people like/as roar water mighty to crash [emph?]
13 Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.
people like/as roar water many to crash [emph?] and to rebuke in/on/with him and to flee from distance and to pursue like/as chaff mountain: mount to/for face: before spirit: breath and like/as wheel to/for face: before whirlwind
14 Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.
to/for time evening and behold terror in/on/with before morning nothing he this portion to plunder us and allotted to/for to plunder us