< Isaya 16 >

1 Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi, Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.
Envoyez, Seigneur, l’agneau dominateur de la terre, de la Pierre du désert à la montagne de la fille de Sion.
2 Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota, ndivyo walivyo wanawake wa Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.
Et il arrivera que, comme un oiseau qui fuit, et des petits qui s’envolent du nid, ainsi seront les filles de Moab au passage de l’Arnon.
3 “Tupeni shauri, toeni uamuzi. Wakati wa adhuhuri, fanyeni kivuli chenu kama usiku. Waficheni watoro, msisaliti wakimbizi.
Prends conseil, convoque une assemblée; fais comme une nuit de ton ombre en plein midi; cache ceux qui fuient; et les errants, ne les trahis pas.
4 Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi; kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.” Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma, aletaye vita atatoweka kutoka nchi.
Mes fugitifs habiteront chez toi; Moab, sois leur retraite contre le dévastateur; car la poussière a trouvé sa fin, le misérable a été consumé; il a défailli, celui qui foulait aux pieds la terre.
5 Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa, kwa uaminifu mtu ataketi juu yake, yeye atokaye nyumba ya Daudi: yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki, na huhimiza njia ya haki.
Et dans la miséricorde sera préparé un trône, et il s’y assiéra dans la vérité, dans le tabernacle de David, un roi jugeant, et recherchant ce qui est juste, et rendant une prompte justice.
6 Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu, kiburi chake na ufidhuli wake, lakini majivuno yake si kitu.
Nous avons appris l’orgueil de Moab; ce peuple est très orgueilleux; et son orgueil, et son arrogance, et sa fureur, sont plus grands que sa puissance.
7 Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza, wanaiombolezea Moabu kwa pamoja. Wanaomboleza na kuhuzunika kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
C’est pour cela que Moab hurlera à Moab; tous hurleront; à ceux qui se réjouissent sur leurs murailles de briques cuites au feu, annoncez leurs plaies.
8 Mashamba ya Heshboni yananyauka, pia na mizabibu ya Sibma. Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana, ambayo ilipata kufika Yazeri na kuenea kuelekea jangwani. Machipukizi yake yalienea yakafika hadi baharini.
Parce que les faubourgs d’Hésébon sont déserts, et que les maîtres des nations ont coupé la vigne de Sabama; ses jeunes branches sont parvenues jusqu’à Jazer; elles se sont répandues çà et là dans le désert; ses rejetons ont été laissés, ils ont passé au-delà de la mer.
9 Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo, kwa ajili ya mizabibu ya Sibma. Ee Heshboni, ee Eleale, ninakulowesha kwa machozi! Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.
À cause de cela, je pleurerai du pleur de Jazer, la vigne de Sabama, je vous enivrerai de mes larmes, Hésébon et Eléalé, parce que sur votre vendange et sur votre moisson est tombée la voix de ceux qui les ont foulées aux pieds.
10 Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka mashamba ya matunda; hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti katika mashamba ya mizabibu; hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni, kwa kuwa nimekomesha makelele.
Et la joie et l’exultation seront enlevées du Carmel, et dans les vignes on n’exultera ni on ne jubilera; il ne foulera pas le vin dans le pressoir, celui qui avait coutume de le fouler; j’ai ôté la voix de ceux qui foulaient.
11 Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi, nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.
À cause de cela, le fond de mon cœur retentira sur Moab, comme la harpe, et mes entrailles sur le mur de briques cuites au feu.
12 Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu, anajichosha mwenyewe tu; anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba, haitamfaidi lolote.
Et il arrivera que, lorsque Moab aura vu qu’il s’est fatigué sur ses hauts lieux, il entrera dans son sanctuaire afin de prier instamment, et qu’il ne pourra rien.
13 Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu.
C’est la parole qu’a dite le Seigneur à Moab anciennement;
14 Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”
Et maintenant le Seigneur a parlé, disant: Dans trois ans, comptés comme les années d’un mercenaire, la gloire de Moab sera enlevée avec tout son peuple nombreux; et il sera laissé petit et faible, et nullement nombreux.

< Isaya 16 >