< Isaya 16 >

1 Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi, Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.
Send ye the lambs to the ruler of the land, From Selah through the wilderness To the mount of the daughter of Zion!
2 Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota, ndivyo walivyo wanawake wa Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.
For as a wandering bird, As a forthdriven nest, So shall be the daughters of Moab At the fords of Arnon; [[saying, ]]
3 “Tupeni shauri, toeni uamuzi. Wakati wa adhuhuri, fanyeni kivuli chenu kama usiku. Waficheni watoro, msisaliti wakimbizi.
“Offer counsel; give decision, Make thy shadow at noonday like the darkness of night. Hide the outcasts; Betray not the fugitives.
4 Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi; kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.” Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma, aletaye vita atatoweka kutoka nchi.
Let my outcasts dwell with thee, [[O Zion!]] Be thou to them a covert from the spoiler! For the extortion is at an end, The spoiling ceaseth. The oppressors are consumed from the land.
5 Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa, kwa uaminifu mtu ataketi juu yake, yeye atokaye nyumba ya Daudi: yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki, na huhimiza njia ya haki.
Then shall your throne be established through mercy, And upon it shall sit in the house of David A judge searching for justice, and prompt in equity.”
6 Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu, kiburi chake na ufidhuli wake, lakini majivuno yake si kitu.
“We have beard of the pride of Moab; he is very proud; His haughtiness, and his pride, and his insolence, His vain boastings.”
7 Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza, wanaiombolezea Moabu kwa pamoja. Wanaomboleza na kuhuzunika kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
Therefore shall Moab howl for Moab; Every one shall howl; For the ruins of Kir-hares shall ye mourn, In deep affliction.
8 Mashamba ya Heshboni yananyauka, pia na mizabibu ya Sibma. Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana, ambayo ilipata kufika Yazeri na kuenea kuelekea jangwani. Machipukizi yake yalienea yakafika hadi baharini.
For the fields of Heshbon languish, The lords of the nations break down the choicest shoots of the vine of Sibmah, They reached even to Jazer; they wandered into the desert; Her branches were spread out; they crossed the sea.
9 Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo, kwa ajili ya mizabibu ya Sibma. Ee Heshboni, ee Eleale, ninakulowesha kwa machozi! Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.
Therefore I will weep, like Jazer, for the vine of Sibmah; I will water thee with my tears, O Heshbon and Elealah, For upon thy summer fruits, and thy harvest, the war-shout is fallen.
10 Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka mashamba ya matunda; hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti katika mashamba ya mizabibu; hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni, kwa kuwa nimekomesha makelele.
Gladness and joy are driven from the fruitful field, And in the vineyards is no singing nor shouting; The treaders tread out no wine in their vats; I have made the vintage-shouting to cease.
11 Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi, nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.
Therefore shall my bowels sound like a harp for Moab, And my inward parts for Kir-hares.
12 Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu, anajichosha mwenyewe tu; anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba, haitamfaidi lolote.
And it shall come to pass that though Moab present himself, Though he weary himself upon his high places, And go up to his sanctuary to pray, Yet shall he not prevail.
13 Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu.
This is the word which Jehovah spake concerning Moab of old.
14 Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”
But now saith Jehovah: Within three years, like the years of a hireling, The glory of Moab shall be put to shame, With all his great multitude; And the remnant shall be very small, and without strength.

< Isaya 16 >