< Isaya 16 >
1 Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi, Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.
Sender Landets Hersker Lam fra Sela gennem Ørken til Zions Datters Bjerg.
2 Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota, ndivyo walivyo wanawake wa Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.
Og det skal ske, at ligesom en Fugl, udjaget af Reden, flagrer hid og did, saa skulle Moabs Døtre komme til Arnons Færgesteder.
3 “Tupeni shauri, toeni uamuzi. Wakati wa adhuhuri, fanyeni kivuli chenu kama usiku. Waficheni watoro, msisaliti wakimbizi.
Giv Raad, hjælp til Ret, gør din Skygge som Natten midt om Middagen, skjul de fordrevne, forraad ikke den, som flyr!
4 Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi; kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.” Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma, aletaye vita atatoweka kutoka nchi.
Lad mine fordrevne faa Herberge hos dig, Moab! vær dem et Skjul imod Ødelæggeren; thi Undertrykkeren er borte, Ødelæggelsen faar Ende, og de, som nedtraadte andre, skulle omkomme af Landet.
5 Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa, kwa uaminifu mtu ataketi juu yake, yeye atokaye nyumba ya Daudi: yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki, na huhimiza njia ya haki.
Og der skal beredes en Trone ved Miskundheden, og en skal sidde derpaa i Sandheden, i Davids Paulun, en, som skal dømme og spørge efter Ret og haste efter Retfærdighed.
6 Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu, kiburi chake na ufidhuli wake, lakini majivuno yake si kitu.
Vi have hørt om Moabs Hovmod, han er saare hovmodig, ja, om hans Stolthed og hans Hovmod og hans Grumhed, hans tomme Pral.
7 Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza, wanaiombolezea Moabu kwa pamoja. Wanaomboleza na kuhuzunika kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
Derfor skal Moab hyle over Moab, de skulle alle sammen hyle; over Kir-Hareseths Grundvolde skulle I sukke, aldeles modfaldne.
8 Mashamba ya Heshboni yananyauka, pia na mizabibu ya Sibma. Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana, ambayo ilipata kufika Yazeri na kuenea kuelekea jangwani. Machipukizi yake yalienea yakafika hadi baharini.
Thi Hesbons Marker ere henvisnede, paa Vintræet i Sibma have Folkenes Herrer knust de ædle Ranker, som naaede til Jaeser og forvildede sig ind i Ørken; dens Kviste, som bredte sig ud, ere komne over Havet.
9 Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo, kwa ajili ya mizabibu ya Sibma. Ee Heshboni, ee Eleale, ninakulowesha kwa machozi! Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.
Derfor vil jeg græde med Jaesers Graad over det Vintræ i Sibma, jeg vil væde dig, Hesbon og Eleale, med min Graad; thi over din Sommerfrugt og over din Høst faldt Krigsskriget ind.
10 Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka mashamba ya matunda; hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti katika mashamba ya mizabibu; hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni, kwa kuwa nimekomesha makelele.
Og Glæde og Fryd er veget bort fra den frugtbare Mark, og man synger ikke i Vingaardene, raaber ej heller med Glæde; Persetræderen træder ikke Druer i Perserne, Frydeskrig har jeg ladet høre op.
11 Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi, nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.
Derfor bruser mit Inderste over Moab som en Harpe, og mit Hjerte over Kir-Heres.
12 Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu, anajichosha mwenyewe tu; anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba, haitamfaidi lolote.
Og det sker, naar Moab lader sig se og er træt af at ofre paa Højen, da vil det komme til sin Helligdom for at bede og skal ikke kunne.
13 Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu.
Dette er det Ord, som Herren har talt imod Moab den Gang;
14 Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”
men nu har Herren talt og sagt: Om tre Aar, som en Daglønners Aar, da skal Moabs Herlighed med al den store Mængde være ringeagtet, og der skal blive en Levning tilbage, liden, ringe og afmægtig.