< Isaya 15 >

1 Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
Moab périra pendant la nuit; c'est la nuit que périront les murs de Moab.
2 Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
Affligez-vous sur vous-mêmes; car Dibon, où était votre autel, périra. Montez-y pour pleurer sur Nabau, ville des Moabites. Poussez des cris de douleur; là toutes les têtes sont chauves, là tous les bras sont coupés;
3 Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
Dans les rues ceignez-vous de cilices, pleurez sur les terrasses, sur les places et dans les faubourgs; gémissez tous et pleurez.
4 Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
Ésebon et Éléalé ont jeté des cris, et jusqu'à Jassa leur clameur a été entendue; c'est pourquoi les reins de Moab crient, et son âme va s'instruire.
5 Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
Moab crie en son cœur jusqu'à Ségor; comme une génisse de trois ans sur la montée de Luith, ainsi vers toi, vaine idole, ils monteront pleurant par la voie d'Aroniim; ils crieront misère et désolation.
6 Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
L'eau de Nemrim sera tarie, et son gazon sèchera, et l'herbe n'y verdira plus.
7 Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
Est-ce que Moab s'attend à être sauvé? Je conduirai les Arabes dans sa vallée, et ils la prendront.
8 Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
Les cris de Moab retentissent jusqu'à ses frontières, et celles mêmes d'Agalim et ses hurlements vont jusqu'au puits d'Élim.
9 Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.
L'eau de Dimon sera pleine de sang; car je conduirai les Arabes sur Dimon, et j'anéantirai la semence de Moab, Ariel et les restes d'Adama.

< Isaya 15 >