< Isaya 15 >

1 Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
Oracle sur Moab. Oui, dans la nuit où elle a été saccagée, Ar-Moab a été ruinée! Dans la nuit où elle a été saccagée, Kir-Moab a été ruinée!
2 Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
On monte au temple de Chamos et à Dibon, aux hauts-lieux, pour pleurer; sur Nebo et Médéba, Moab se lamente, Toute tête est rasée, toute barbe est coupée.
3 Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
Dans ses rues, ils se revêtent de sacs; sur ses toits et sur ses places publiques; tous poussent des hurlements, fondent en larmes.
4 Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
Hésebon et Eléalé jettent des cris; on entend leur voix jusqu'à Jahas. C'est pourquoi les guerriers de Moab se lamentent, et son âme est tremblante.
5 Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
Mon cœur gémit sur Moab; ses défenseurs sont déjà à Ségor, à Eglath-Schelischiah. Oui, la montée de Luhith, on la gravit en pleurant; et sur le chemin de Horonaïm, on pousse des cris de détresse.
6 Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
Car les eaux de Nimrim sont taries, l'herbe est desséchée, le gazon est détruit, il n'y a plus de verdure.
7 Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
Ce qu'ils ont pu sauver et leurs provisions, ils les transportent au delà du torrent des Saules.
8 Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
Car les cris ont fait le tour du territoire de Moab; ses hurlements retentissent jusqu'à Eglaïm, ses hurlements jusqu'à Béer-Elim;
9 Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.
car les eaux de Dimon sont pleines de sang. Car je ferai venir sur Dimon un surcroît de malheur, un lion aux réchappés de Moab, à ce qui sera resté dans le pays.

< Isaya 15 >