< Isaya 15 >
1 Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
The burden of Moab. For in a night Ar of Moab is laid waste, and brought to nothing. For in a night Kir of Moab is laid waste, and brought to nothing.
2 Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
They have gone up to Bayith, and to Dibon, to the high places, to weep. Moab wails over Nebo, and over Medeba. On all their heads is baldness. Every beard is cut off.
3 Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
In their streets they gird themselves with sackcloth. On their housetops, and in their broad places, everyone wails, weeping abundantly.
4 Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
And Heshbon cries out, and Elealeh. Their voice is heard even to Jahaz. Therefore the armed men of Moab cry aloud. His soul trembles within him.
5 Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
My heart cries out for Moab. Her nobles flee to Zoar, to Eglath-shelishi-yah. For they go up with weeping by the ascent of Luhith. For they raise up a cry of destruction in the way of Horonaim.
6 Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
For the waters of Nimrim shall be desolate, for the grass is withered away. The tender grass fails. There is no green thing.
7 Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
Therefore the abundance they have gotten, and that which they have laid up, they shall carry away over the brook of the willows.
8 Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
For the cry has gone round about the borders of Moab, the wailing of it to Eglaim, and the wailing of it to Beer-elim.
9 Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.
For the waters of Dimon are full of blood. For I will bring yet more upon Dimon, a lion upon those of Moab who escape, and upon the remnant of the land.